Skip to main content

Posts

Showing posts from February 25, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Huyu Ndio Waziri Ofisi ya Rais Anashughulikia Vijana

 Kijana huyu alizaliwa Julai 4, 1983 huko Mtwara. Akasoma shule ya msingi Shangani iliyopo Mtwara Mjini kuanzia 1992 hadi 1998. Mtihani wa darasa la Saba akashika nafasi ya tatu kiMkoa. Akachaguliwa kujiunga kidato cha kwanza shule ya sekondari ya vipaji maalumu Kibaha, Pwani. Mwaka 2000 akafanikiwa kuingia kumi bora mtihani wa kidato cha pili kwa kanda ya mashariki, akaongoza masomo mawili ikiwemo Hisabati. Mwaka 2002 akahitimu kidato cha Nne kwa kupata alama “A” katika masomo tisa kati ya kumi aliyofanya katika mtihani wa taifa. Baraza la Mitihani “NECTA” likamtangaza Joel kuwa Mwanafunzi bora kitaifa. Akachaguliwa kuendelea sekondari Kibaha, Mchepuo wa PCB. Akahitimu kidato cha sita na kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kusomea shahada ya Biashara na Uongozi. Baadae akasoma stashahada ya juu ya Diplomasia ya Uchumi (post-graduate in economic diplomacy). Badae akasoma shahada ya uzamili ya maendeleo na uhusiano wa kimataifa (International cooperation and development). Anaju...

Waziri Kombo Asisitiza Ufanisi na Uadilifu kwa Watumishi wa Wizara

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasisitiza watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi, uadilifu na kufuata sheria, Kanuni na miongozo ya utumishi wa umma. Amesema hatua hiyo itaendelea kukuza weledi katika kazi kwa watumishi wa wizara, na hivyo kujenga na kuimarisha taswira  ya wizara ndani na nje ya nchi. Waziri Kombo ametoa rai hiyo alipokutana na watumishi wa wizara katika kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma. “Leo tumekutana wote kwa mara ya kwanza, watumishi wenzangu hamna budi kufanya kazi kwa ufanisi na mzingatie maadili na kufuata sheria, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma ili kujenga na kuimarisha taswira ya Wizara yetu ndani na nje ya Nchi na kulinda maslahi mapana ya nchi” alisema Mhe. Waziri. Amebainisha kuwa watumishi wana dhamana kubwa ya kusimamia na kutekeleza diplomasia ya uchumi, jambo linalohitaji uzalendo katika kutekeleza ma...

Waziri Sangu: Mahusiano Mema Msingi wa Umoja Wa Taifa

✅ Ahimiza Mshikamano katika kujenga Tanzania Imara Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu amesisitiza umuhimu wa kudumisha mahusiano mema ili kuimarisha umoja wa Taifa na kuchochea maendeleo endelevu nchini. ‎Mhe. Sangu amesema hayo wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Wadau wa Mahusiano kilichofanyika tarehe Februari 24, 2026 katika Halmashauri ya Sumbawanga mkoani Rukwa. Aidha, amesema kuwa uwepo wa mahusiano imara miongoni mwa Watanzania ni nguzo muhimu ya kudumisha amani, umoja na mshikamano wa Taifa. ‎Ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kuratibu na kuimarisha mahusiano baina yake na makundi mbalimbali ya kijamii ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa kielelezo cha utulivu barani Afrika. ‎Amesema kuwa, sifa ya Mtanzania ambayo ni miongoni mwa sifa kuu zinazomtambulisha ni mahusiano mazuri yanayobebwa na misingi mikuu mitatu, msingi wa kwanza ni mila na desturi za nchi, ambapo, Nchi yetu ina historia ndefu ya ushirikiano na utani kati ya ma...

Washindi 9 wa Mawazo Bunifu Watunukiwa Tuzo

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa Tuzo za ubunifu kwa washindi 9 waliotoa mawazo bora zaidi yatakayosaidia kuendelea kuboresha huduma za kodi na kuongeza wigo wa kodi.  Akikabidhi tuzo hizo, vyeti pamoja na hundi kwa washindi hao Februari 25.2026, Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar ameipongeza TRA kwa kuja na Tuzo hizo ambazo zitaongeza ukaribu na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ukusanyaji wa kodi.  Mshindi wa jumla katika tuzo hizo ni Gabriel Mashenene ambaye amepatiwa hundi ya Sh. Milioni 50, washindi watatu wamepatiwa Sh. Milioni 30 kila mmoja huku washindi 5 wakipatiwa Sh. Milioni 20  kwa kila mmoja.

Serikali Yaweka Mkakati wa Kuitangaza Tanzanite na Madini ya Vito Nchini Qatar

■ Ni utekelezaji wa maagizo ya Mh Rais Samia kurudisha heshima ya Tanzanite ■ Mkutano wa wawekezaji na wafanyabiashara wa madini baina ya Nchi mbili kuandaliwa ■ Wafanyabiashara wa madini ya vito kushiriki maonesho ya bidhaa za madini Qatar mwezi April 2026 📍Doha, Qatar. Katika utekelezaji wa ahadi ya kurejesha thamani na hadhi ya madini ya vito ya Tanzanite, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa *Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan* imeweka mkakati thabiti wa kutangaza madini ya Tanzanite nchini Qatar ili kuongeza wigo wa masoko yake na kuvutia uwekezaji na utalii. Hayo yamesemwa leo tarehe 25 Februari, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* alipotembelea Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Qatar na kufanya mazungumzo na watumishi wa ubalozi. "Soko la Tanzanite miaka ya hivi karibuni lilionekana kushuka kidogo na ndiyo maana hata bei imeshuka. Mhe. Rais ameskia kilio cha wachimbaji na wafanyabiashara wa Tanzanite na kutuagiza Wizara...

Ppaa Yaokoa Bilioni 586 Kwa Kukataa Kutoa Tuzo za Zabuni 43

 DODOMA  SERIKALI Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kupitia Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeokoa Shilingi bilioni 586.5 baada ya kuzuia utoaji wa tuzo za Zabuni 43 zilizokuwa zimetolewa kwa wazabuni waliokosa uwezo wa kifedha na sifa za kitaalamu za kutekeleza miradi husika. Hatua hii ni utekelezaji usioridhisha wa miradi ambao ungesababisha upotevu wa fedha za umma na kuchelewesha maendeleo endelevudelevu na stahiki kwa wananchi. Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma leo Februari 25,2026 na Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando, wakati wa mkutano wake na waandishi wa Habari Kuhusu siku.100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Amesema kupitia kitengo cha rufaa, Mamlaka imesajili mashauri 196 yaliyotokana na michakato mbalimbali ya ununuzi wa umma ambapo Kati ya mashauri hayo, zabuni 43 zenye thamani ya Shilingi bilioni 586.5 zimezuiwa kutolewa kutokana na wazabuni husika kutokidhi vigezo vya kifedha na kitaalamu. "Usuluhishi wa migogoro hauwez...