Na Mwanamkuu Mwandoro,Lushoto. Jeshi la polisi mkoani Tanga limemtia mbaroni mtuhumiwa wizi wa mtoto mchanga katika hospitali ya wilaya ya Lushoto aliyefahamika Kwa jina la Habiba Fundi. Akizungumza na waandshi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Juni 21,2026,saa Moja usiku katika kitongoji Cha Gerekaya,Kijiji Cha kwemashai wilayani Lushoto akiwa na mtoto huyo. Mchunguzi amesema Juni 19,majira ya saa Moja jioni mama mzazi wa mtoto huyo Mwanaidi Nyaki ,mkazi wa Kijiji Cha Kwemakame aliripoti kupotelewa na mtoto wake wa siku Moja. Kamanda mchunguzi amesema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mwanamke huyo ambaye hakufahamika Kwa wakati huo alijenga ukaribu na mama mzazi pamoja na ndugu walikuwa wakimuhudumia hospitalini,na baada ya kujenga urafiki na kuaminiwa alitumia fursa hiyo kumchukuwa mtoto huyo mchanga na kumuweka kwenye beseni lenye nguo na kutoweka nae. Aidha kamanda huyo pia aliongeza kuwa aliidanganya f...
Marato tv - Sauti ya Jamii