Skip to main content

Posts

Showing posts from September 4, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

TANZANIA, MAREKANI KUIUNGANISHA AFRIKA KWENYE SEKTA YA AFYA

 *Na John Mapepele – WAF**Washington, D.C.* Serikali ya Tanzania imekubaliana na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C na Serikali ya Marekani kufanya utekelezaji wa kimkakati wa mkataba wa sekta ya afya ulioingiwa hivi karibuni ili kuzinufaisha pande zote mbili,huku wakiifanya Tanzania kuwa muhimili wa uzalishaji na usambazaji dawa na vifaa tiba katika bara la Afrika. Akizungumza katika leo kwenye Mkutano wa Wadau wa Ushirikiano wa Afya kati ya Marekani na Tanzania uliofanyika leo kati ya Serikali ya Tanzania na Chama cha Wafanyabiashara cha Marekani (U.S. Chamber of Commerce) mjini Washington, D.C., na baadaye kufanya kikao viongozi waandamizi Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Waziri wa Afya wa Tanzania, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa, alifafanua kuwa tayari Tanzania imejipanga vema kuhakikisha mkataba unatekelezwa kikamilifu. Akielezea zaidi kuhusu mazingira rafiki ya uwekezaji kwenye sekta ya dawa amesema Tanzania inafanya k...

WATANZANIA 440 WAONDOKA AFRIKA KUSINI KWA HIARI, 192 WAREJEA LEO

Jumla ya Watanzania 440 wameondoka kwa hiari kutoka maeneo mbalimbali nchini Afrika Kusini na kurejea Tanzania, huku Watanzania 192 wakiondoka Jijini Cape Town leo, Septemba 4, 2026, kupitia Shirika la Ndege Tanzania (ATCL). Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, James Bwana, amesema Watanzania hao 192 wanatarajiwa kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo saa nne usiku. Amesema idadi hiyo inafanya jumla ya Watanzania 267 kutoka Cape Town pekee kuwa wameondoka na kurejea Tanzania ndani ya siku mbili, baada ya Watanzania 75 kuondoka jana, Septemba 3, 2026. Watanzania hao 267 wanaungana na Watanzania 173 waliosafirishwa kutoka Durban Agosti 26, 2026, hivyo kufikisha jumla ya Watanzania 440 waliosafiri kwa hiari kutoka Afrika Kusini kurejea Tanzania hadi Septemba 4, 2026. Balozi Bwana amewatakia Watanzania hao safari njema na maisha mema wanaporejea katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MWENGE WA UHURU WATAKA MAJUKWAA YA VIJANA YASHUSHWE HADI VIJIJINI KYERWA

 Na Angela Sebastian  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwango’nda, ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa kuhakikisha majukwaa ya vijana yanashushwa kutoka ngazi ya wilaya hadi kata, vijiji na mitaa, ili kuwawezesha vijana wengi zaidi kupata elimu na taarifa kuhusu fursa zinazotolewa na Serikali. Mwango’nda alitoa agizo hilo wakati akizindua Jukwaa la Vijana katika Wilaya ya Kyerwa, akieleza kuwa majukwaa hayo yamekuwa yakifanya kazi katika ngazi ya wilaya, hivyo ni muhimu viongozi na watendaji wa Halmashauri kuyapeleka karibu zaidi na vijana walioko katika maeneo yao. Alisema hatua hiyo itasaidia kuongeza uelewa wa vijana kuhusu fursa mbalimbali, ikiwemo mikopo na programu za kuwawezesha kiuchumi. “Serikali imeweka nguvu nyingi kwa vijana, na hamasa ya sasa ni kuhakikisha vijana wanajiajiri kupitia vikundi mbalimbali. Serikali iko tayari kuwahangaikia; kinachopungua kwa sasa ni elimu na namna ya kutumia fursa zilizopo. Hivyo viongozi wa Halmashauri w...