Na Mwandishi wetu Jovina Massano. Katibu wa Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Tanzania TWCC Mkoa Wa Mara Anastazia Maximilian ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuiboresha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuweka mfumo bora wa huduma za mapato hapa nchini. Akizungumza mwandishi wetu katibu huyo amesema mpango wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) wa kuja na Mfumo Jumuishi wa Utawala wa Mapato ya Ndani(IDRAS) utawezesha kuokoa muda kwa wafanyabiashara sambamba na kuondoa usumbufu kutoka sehemu moja kwenda nyingine ikiwemo kupunguza ghalama kwa walipa Kodi. "Mfumo huu unamanufaa makubwa kwetu sisi wafanyabiashara kwa kuwa umetuondolea adha ya kutembea na nyaraka wakati wa kuwasilisha ritani na kulipia Mapato hii inatusaidia kuepuka upotevu wa nyaraka lakini pia utatuwezesha kujihudumia mwenyewe kupitia mfumo huo wa IDRAS"amesema Anastazia. Aidha ameipongeza TRA kwa kutambua thamani ya lugha ya Kiswahili kwa kuwezesha kuwa mojawapo ya lugha zinazotumika katika Mfumo wa I...
Marato tv - Sauti ya Jamii