Skip to main content

Posts

Showing posts from April 10, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri wa Ulinzi na Jkt Akutana na Kufanya Mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) tarehe 09 April, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mheshimiwa Guy Kabombo Muadiamvita aliyefanya ziara ya kikazi nchini Tanzania. Mazungumzo hayo ya Kikazi baina ya Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yalifanyika katika Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Kikombo jijini Dodoma, yalilenga kuimarisha ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu na kihistoria baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika Diplomasia ya Ulinzi.  Katika kikao hicho, Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt Rhimo Nyansaho amemhakikishia Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kongo,utayari wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan  kupitia Wizara ya Ulinzi na JKT,  kushi...

Rpc Mutafungwa Awatoa Hofu Ukerewe, Aonya Kujichukulia Sheria Mkoani

Na Dawati la Habari Polisi; Mwanza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewatoa hofu wakazi wa Wilaya ya Ukerewe kufuatia kuibuka kwa viashiria vya uvunjifu wa amani baada ya kutokea kwa tukio la kijana mmoja, Leonard Mganga (44), mkazi wa Kitongoji cha Kabo, Kijiji cha Nampisi na kujeruhi waumini wawili wa kanisa katoliki. Mtuhumiwa huyo aliingia Kanisa la Bikira Maria Mama wa Tumaini Jema, Parokia ya Kagunguli, Jimbo Katoliki la Bunda kupitia mlango mdogo kulia mwa jengo hilo na kuwashambulia kwa panga waumini wawili baada ya kutolewa nje, hali iliyozua taharuki kubwa wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya Pasaka. Tukio hilo lilitokea tarehe 5 Aprili, 2026, majira ya saa 1:30 asubuhi, ambapo kijana huyo aliingia kanisani akiwa amebeba mfuko uliokuwa na panga alilolitumia kuwashambulia waumini hao. Mtuhumiwa huyo alipoteza maisha kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kushambuliwa na waumini pamoja na wananchi wenye hasira waliokuwepo eneo la tukio. Akizungumza na wananchi wa ...

Serikali Yafafanua Matumizi ya Mkopo wa Trilioni 1.2 Kujenga Upya Hospitali ya Taifa Muhimbili

Na Shaban Juma, WAF – Dodoma Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, amesema Serikali inatarajia kujenga upya Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia mkopo wa shilingi trilioni 1.2, badala ya kufanya ukarabati wa majengo yaliyopo sasa. Dkt. Samizi ametoa ufafanuzi huo bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu hoja ya Mbunge wa Sumbawanga, Mhe. Aeshi Hillary, aliyehoji kuhusu matumizi ya mkopo huo uliotengwa kwa ajili ya hospitali hiyo. Amesema uamuzi wa kujenga hospitali mpya unatokana na hali ya majengo ya sasa kuwa yamechoka na kusambaa katika maeneo mbalimbali, hali inayopunguza ufanisi wa utoaji huduma na kushindwa kukidhi viwango vinavyohitajika kwa hospitali ya taifa. Ameeleza kuwa kupitia mkopo huo, Serikali itatekeleza ujenzi wa hospitali ya kisasa pamoja na usimikaji wa mitambo ya tiba ya kisasa, hatua itakayoongeza ubora wa huduma za afya na kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi. Aidha, amebainisha kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa majengo mapya ya hospitali yenye jumla ya ...

Serikali imetoa ufafanuzi kupinga uongo wao

  Serikali inapenda kutoa ufafanuzi kwa umma kufuatia taarifa potofu iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuhusu uteuzi wa Mbunge uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 02 Aprili 2026 chini ya Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni sahihi kuwa kabla ya uteuzi huo, Mheshimwa Angela Kizigha alikuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA). Hata hivyo, kwa mujibu wa Ibara ya 51(3)(c) ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mbunge wa EALA hukoma kuwa Mbunge endapo atateuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Nchi Mwanachama. Kutokana na masharti hayo, ubunge wa EALA kwa Mheshimiwa Angela Kizigha na Waheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe na James Milya ulikoma baada ya kuteuliwa/kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, Ibara ya 50 ikisomwa pamoja na Ibara ya 52 ya Mkataba inatoa mamlaka kwa Bunge la Nchi Mwanachama kujaza nafasi zilizo wazi katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Ma...

Minara 758 yazinduliwa huku wananchi milioni 8.5 kunufaika na huduma ya mawasiliano

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ameielekeza Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuhakikisha kuwa miundombinu ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano inakamilika kufika katika wilaya zote nchini ifikapo mwezi Desemba mwaka huu kama ilivyopangwa. Rais Samia ametoa maelekezo hayo leo jijini Dodoma wakati akizindua minara 758 ya mawasiliano pamoja na maunganisho ya mkongo katika wilaya 85, hatua iliyowezesha pia kukabidhi rasmi Mkongo wa Mawasiliano Serikalini. Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha huduma za mawasiliano zinafika hadi ngazi ya kata na vitongoji, ili kila Mtanzania, bila kujali alipo, anufaike na fursa za uchumi wa kidijitali. “Teknolojia ya habari na mawasiliano ni sekta ya kimkakati inayochochea ajira, kuongeza tija katika uzalishaji na kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Serikali imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya mawasiliano,” amesema Rais Samia. Ameongeza kuwa Mkongo wa Taifa umeunganisha mikoa yo...

Waziri Mkuu Aongoza Kikao Cha Mawaziri na Makatibu Wakuu

  Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiongoza Kikao cha Kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, TAMISEMI na Wizara ya Elimu Sanyansi na Teknolojia kuhusu utekelezaji wa Elimu Msingi ya Lazima kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma, Aprili 10, 2026.

Rais Ameniteua Kuwa Daraja Kati ya Dini na Serikali- Katambi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi amefanya Kikao Kazi na Viongozi wa Dini nchini huku akiwaeleza Viongozi hao kuwa ameteuliwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa daraja Kati ya Viongozi wa Dini na Serikali ambapo amewaambia milango iko wazi kwa viongozi hao kuongea na kushauriana na serikali ikiwemo utoaji wa maoni mbalimbali kwa serikali lengo ikiwa kudumisha tunu ya Amani na kuhakikisha kuwepo kwa Utulivu nchini. Amezungumza hayo leo,jijini Dar es Salaam katika kikao kilichohudhuriwa  pia na Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Maduhu Kazi na Msajili wa Jumuiya,Emmanuel Kihampa ambapo Viongozi wa Dini takribani 45 wakiwa wamehudhuria Mkutano huo. *“Nimebeba dhamana hii kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan na Nchi yetu kuwa kiungo muhimu cha mahusiano, Usalama, amani na maendeleo au Daraja la kuvusha mema.Hii Wizara(Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)kimsingi ni dhamana yake kwasababu yeye ndio Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vyote vya Ulinzi n...