Skip to main content

Posts

Showing posts from August 23, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MWANANYAMALA

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza leo Jumapili, Agosti 23, 2026, katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam, kukagua hali ya utoaji wa huduma kwa wananchi. Alipowasili hospitalini hapo, Dkt. Mwigulu ametembelea wodi mbalimbali, zikiwemo Wodi ya Mama na Mtoto na Wodi ya Upasuaji, ambako amezungumza na wagonjwa pamoja na ndugu zao na kusikiliza maoni yao kuhusu huduma zinazotolewa hospitalini hapo na changamoto wanazokabiliana nazo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wanaopata huduma hospitalini hapo wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Serikali kwa ujumla kwa kuendelea kuboresha huduma za afya na mazingira ya utoaji wa huduma hospitalini hapo. Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila; Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Saad Mtambule; pamoja na viongozi wa Hospitali hiyo.

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MWANANYAMALA

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza leo Jumapili, Agosti 23, 2026, katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam, kukagua hali ya utoaji wa huduma kwa wananchi. Alipowasili hospitalini hapo, Dkt. Mwigulu ametembelea wodi mbalimbali, zikiwemo Wodi ya Mama na Mtoto na Wodi ya Upasuaji, ambako amezungumza na wagonjwa pamoja na ndugu zao na kusikiliza maoni yao kuhusu huduma zinazotolewa hospitalini hapo na changamoto wanazokabiliana nazo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi wanaopata huduma hospitalini hapo wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Serikali kwa ujumla kwa kuendelea kuboresha huduma za afya na mazingira ya utoaji wa huduma hospitalini hapo. Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila; Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Saad Mtambule; pamoja na viongozi wa Hospitali hiyo.

MSHINDI MAONESHO YA ELIMU,UJUZI NA UBUNIFU KUIWAKILISHA TANZANIA KIMATAIFA

 Na Mwanamkuu Mwandoro, Tanga. Washindi kupitia maonesho ya Elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea kufanyika kitaifa mkoani Tanga wanatarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika maonesho ya kidunia kwenda kuonesha ujuzi ,ubunifu na maarifa yao. Hayo yameelezwa na katibu mtendaji kutoka baraza la Taifa la elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET) Mwajuma Lingwanda wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho hayo ambapo amesema jumla ya washiriki 49 waliopatikana kwenye mchujo uliofanyika katika ngazi ya Kanda watashindanishwa kwenye vipengele 9 ambapo kila mshidi atakata tiketi ya kwenda kuiwakilisha Tanzania kimataifa. "Mashindano haya yalianza katika ngazi ya Kanda ambapo tulikiwa na washiriki katika maeneo 9 ya ujuzi na baada ya hapo tumefikia kwenye maonesho ya kitaifa na tuna washiriki 49 kutoka kwenye taasisi mbalimbali waamuzi wako tayari wale watakaofanikiwa kufaulu na kuwa washindi wa kwanza watapata nafasi ya kushiriki kwenye mashindano ya k...

MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA (TEA),KUKUZA NDOTO ZA VIJANA

 Na Mwanamkuu Mwandoro , Tanga. MWANAFUNZI wa amali ya upishi kutoka shule ya Sekondari ya wasichana ya Korogwe iliyopo mkoani Tanga Ntuli Danken Mwanganga ameanza kuona mwanga hadi kutamani kutimiza ndoto ya kuwa mfanyabiashara mkubwa wa chakula ujuzi ambao alianza kujifunza kutoka mikononi mwa Mama yake mzazi aliyekuwa mama ntilie akihitaji kuiboresha zaidi biashara hiyo.  Akizungumza katika maadhimisho ya wiki ya kitaifa ya elimu ujuzi na ubunifu yanayoendelea kufanyika kitaifa mkoani Tanga Ntuli ameishukuru mamlaka ya elimu Tanzania (TEA)kwa kuwapatia vifaa ambavyo vimekuwa msaada mkubwa katika kujifunza kwao kwani vimewaongezea uelewa tofauti na awali walipokuwa wakijifunza kwa nadharia pekee. "Mwanzo wakati hatujaletewa vifaa ilikiwa shida sana kujifunza tulikiwa tunasoma tu na kuelekezwa hata matokeo yetu hayakuwa mazuri lakini sasa tunawashukuru sana TEA kwa kutuletea vifaa tunajifunza kwa vitendo na kutumia vifaa" "Nimependa na nimechagua somo la upishi ...

CHATANDA: UTHABITI WA RAIS SAMIA UMEKAMILISHA MRADI WA UMEME WA JNHPP

 NA: MWANDISHI WETU Historia kubwa imeandikwa Tanzania. Hii ni kufuatia kukamilika kwa mradi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere (JNHPP), chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 katika eneo la mradi, wilayani Rufiji, mkoani Pwani. Kukamilisha kwa mradi huo uliogharimu shilingi trilioni 7.452, kunachochea moja kwa moja maendeleo ya shughuli za kijamii na kiuchumi kupitia uzalishaji wa nishati ya umeme ambayo ni muhimu katika shughuli hizo. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi mradi huo Agosti 22, 2026 wilayani Rufiji.  Akitoa maoni yake kuhusiana na uzinduzi wa mradi huo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, Mary Chatanda, amesema kama Rais Dk. Samia asingekuwa thabiti katika uongozi wake, mradi huo usingekamilika. "Rais Dk. Samia alipoingia madarakani mwaka 2021, alikuta mradi huu umefikia utekelezaji wa asilimia 33, lakini ndani ya miaka mitano ya uongozi wake, mradi huo umekamilika wote na unazalisha megawati 2,115 za umeme...

BRELA YAWAHIMIZA WABUNIFU KUSAJILI BUNIFU ZAO MAPEMA KUDHIBITI BIDHAA BANDIA

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umesema kuwa hatua ya mbunifu kusajili bidhaa au kazi aliyoibuni ni njia pekee na madhubuti ya kuitofautisha kazi hiyo na bidhaa bandia zinazoweza kuingizwa sokoni na wajanja kwa lengo la kujinufaisha isivyo halali. Wito huo umetolewa na Afisa Usajili kutoka BRELA, Benedickson Willson, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara mkoani Tanga. Willson amesema BRELA imeshiriki katika maonyesho hayo, yanayofanyika kuanzia Agosti 15 hadi 24 mwaka huu, kwa lengo la kuwafikia wabunifu na kuwaelimisha umuhimu wa kusajili kazi zao ili kupata haki ya kipekee ya kuzitumia na kuzilinda dhidi ya matumizi yasiyoidhinishwa. Akifafanua kuhusu ulinzi huo, Afisa huyo alisema kuwa usajili wa alama ya biashara na huduma humwezesha mmiliki kulinda chapa yake, huku akisisitiza kuwa ukiwa umesajili alama yako un...

TANZANIA YAFUNGUA MILANGO YA UJUZI DUNIANI KUPITIA WORLDSKILLS

Mkurugenzi wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Fredrick Salukele amesema ushiriki Tanzania katika mashindano ya ujuzi ya WorldSkills umefungua fursa mpya za kimataifa kwa vijana wenye ujuzi, huku tayari washiriki wawili wakikubaliwa kwenda Shanghai, China kama waangalizi wa Mashindano ya WorldSkills International 2026. Akizungumza wakati wa Mashindano hayo yanayoendelea jijini Tanga, Selukele amesema vijana hao wanatoka katika fani za mtandao wa vitu na urembo tiba, hatua inayoonesha kuwa ujuzi wa Tanzania umeanza kutambulika kimataifa. "Baada ya matokeo ya mashindano ya kitaifa kutangazwa, Tanzania itawasilisha washindi kwa WorldSkills ili kuitangazia dunia kuwa nchi yetu ina taasisi zinazozalisha wahitimu wenye ujuzi unaokidhi viwango vya kimataifa,"amesema. Amesema kuonekana katika majukwaa ya WorldSkills kunawaongezea vijana nafasi za ajira za kimataifa, huku Serikali ikilenga kuanzisha mfumo wa vyeti vinavyotambulik...