Skip to main content

Posts

Showing posts from February 24, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Chemba ya Taifa ya Biashara Kuunganisha Mifumo na Serikali

Na mwandishi wetu Jovina Massano. Chemba ya Taifa ya Biashara (TNCC) ambayo hapo awali ilifahamika kama TCCIA kuunganisha mifumo  yake na Serikali ili iweze kusomana  na kubadilishana taarifa kwa ufanisi hapa nchini. Hatua hiyo inalenga kupunguza urasimu katika utoaji wa huduma na kuimarisha mazingira ya Biashara kupitia maboresho ya teknolojia hiyo. Katika kuhakikisha mageuzi hayo yanafanikiwa kwa kiasi kikubwa, Chemba ya Taifa ya Biashara(TNCC) imezindua mafunzo ya wiki moja mkoani Mbeya yanayohusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji wa Vyeti vya Uasili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP). Mafunzo hayo yanahusisha mikoa 14 ikiwemo Ruvuma, Morogoro na Dodoma, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi wa TNCC pamoja na wafanyabiashara ili waweze kutumia mfumo huo kwa ufanisi. Mfumo huo utaongeza uwazi, kupunguza urasimu na kuharakisha utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara, huku ukiunganisha moja kwa moja mifumo ya TNCC na Serikali kwa ufanisi zaidi. Akiongea ka...

Rais Samia Alipa Nguvu Jeshi La Ulinzi Wa Wananchi Tanzania (Jwtz )

 DODOMA. Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema serikali itaendelea kuliwezesha Jeshi la Tanzania kuwa na mazingira bora ya kazi ili liwe tayari wakati wote kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi pamoja na kulinda amani hali itakayo saidia kukuwa kwa uchumi. Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Februari 24, 2026, wakati akizindua jengo la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa katika eneo la Kikombo, jijini Dodoma, ambapo ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi huo imekamilika kwa gharama ya takribani shilingi bilioni 121, fedha zilizotolewa na serikali.  Kadhalika amesema kuwa dhamira ya kuliwekea mazingira bora Jeshi la Tanzania inatokana na dhana kwamba Taifa lolote linalotaka kuheshimiwa duniani halina budi kuwekeza katika taasisi imara za kulinda uhuru, mipaka, rasilimali na watu wake.  “Majengo haya mapya ni nyenzo tu za kutekeleza majukumu yetu, lakini nguvu ya jeshi haitokani na majengo wala vifaa peke yake,” amesema Rais Samia. Akit...

Dkt. Mwigulu Akagua Maendeleo Ujenzi wa Mradi wa Stendi ya Mabasi, Arusha.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 24, 2026 amekagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani unaotekelezwa katika eneo la Bondeni City katika Halmashauri ya Jiji la Arusha.  Mradi huo ambao utagharimu shilingi bilioni 14.3 una lengo la kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji na kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Arusha. Mradi huo ambao unatarajiwa kukamilika Mwezi Mei 2026 umefikia asilimia 49.

Tanzania kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na Singapore

Na Mwandishi Wetu TANZANIA imeahidi kuimarisha ushirikiano wa sekta binafsi ya Tanzania na Shirikisho la Biashara la Singapore kama mkakati wa kukuza kiwango cha biashara baina ya mataifa hayo. Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Viwanda, Denis Londo, wakati akizungumza na Balozi wa Singapore nchini Tanzania, Balozi Douglas Foo. Londo alisema ushirikiano huo utasaidia kukuza biashara na uwekezaji, hasa inayohusisha biashara ndogo na za kati. “Tanzania iko tayari kufanya kazi kwa karibu na Singapore ili kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji, kukuza uongezaji thamani, kubadilisha bidhaa nje ya nchi, na kuiweka Tanzania kama kitovu cha kimkakati cha uzalishaji na usambazaji wa bidhaa EAC, SADC, na COMESA,” alisema “Tunaposhiriki katika majadiliano haya tunatazamia kubadilishana mawazo kuhusu hatua za vitendo ili kutafsiri maono yetu ya pamoja kuwa miradi na ushirikiano madhubuti ambao utatoa manufaa yanayoonekana kwa watu wetu,” alisema. Alisema Singapore imepiga hatua kubwa kiuchumi ...

Bodi za Maji Amkeni, Mfanye Kazi - Dkt. Mwigulu

*Akemea upotevu wa maji, uwepo wa vishoka WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wajumbe wa Bodi za Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini waamke na wasimamie majukumu yanayohusu sekta ya maji. "Tukitoka hapa twende tukatimize wajibu wetu wa kusimamia masuala ya maji. Someni upya kazi za Bodi, ninyi si wasaidizi wa Wakurugenzi. Bodi inapaswa ijue jambo lao kabla hata halijafika kwa Mheshimiwa Waziri," amesisitiza.  Waziri Mkuu ametoa wito huo leo (Jumanne, Februari 24, 2026) wakati akizungumza na washiriki wa mkutano wa siku mbili wa Bodi za Wakurugenzi wa Mamlaka za Maji nchini unaofanyika katika hoteli ya Ngurdoto, jijini Arusha. Mkutano huo wa kitaifa unawakutanisha viongozi wakuu wa usimamizi wa Mamlaka 85 za maji nchini. Waziri Mkuu amesema moja ya maeneo wanapaswa kusimamia ni kukomesha upotevu wa maji. “Leo bado tuna maeneo mengi yenye upotevu mkubwa wa maji. Twendeni tukakague miundombinu yetu, tukomeshe kitu kinaitwa upotevu wa maji. Kuna maeneo maji ya...