Skip to main content

Posts

Showing posts from December 22, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kagera Waanza Kujinoa Kwa Bima ya Afya Kwa Wote

  Angela Sebastian ;Bukoba Viongozi wa sekta mbalimbali za Serikali,dini na watoa huduma za Afya mkoani Kagera wamejengewa uelewa juu ya utekelezaji wa sheria ya mfuko wa bima ya Afya kwa wote, ikiwa ni kuanza kutekelezaji wa ahadi ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ya siku 100 aliyoitoa wakati wa kampeini za uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Mafunzo hayo yametolewa leo katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa kagera ambapo wamesisitizwa kutoea elimu juu ya sheria hiyo kwa nguvu zote kwa wananchi huku wahudumu wa Afya wakitakiwa kuondokana na mazoea katika utoaji wa huduma. Said Makola ni mratibu wa mpango wa Elimu ya Bima ya Afya kwa Wote  kutoka Wizara ya Afya akizungumza katika mafunzo hayo  alisema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya wanao wajibu wa kutoa miongozo na tafsiri ya sheria ya bima ya afya pamoja na kanuni zake ili ziweze kutekelezwa kwa urahisi katika mikoa yote Tanzania Bara. Alisema zaidi kaya laki  9.3 sawa na asilimia 23.7 kwa hawamu ya kwanza zimetambuliwa...

Serikali Kujenga Mtambo wa Kuchenjua Dhahabu Mwakitolyo Shinyanga

■ Ni maelekezo ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan ▪️Zaidi ya tani 100 - 120 kuchenjuliwa kwa siku ■ Makundi ya vijana na wanawake kupatiwa leseni kupitia programu ya MBT ■ Leseni zisizoendelezwa kufutwa kwa mujibu wa sheria ■ Aelekeza Wachimbaji kufuata kanuni za usalama za uchimbaji kuepuka madhara *Mwakitolyo, Shinyanga Kufuatia maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, *Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan* ya kuwasimamia wachimbaji wadogo, Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ipo mbioni kuanza ujenzi wa mtambo wa kuchenjua madini ya dhahabu mkoani Shinyanga. Hayo yameelezwa leo tarehe 22 Desemba, 2025 na Waziri wa Madini, *Mh. Anthony Mavunde* alipofanya ziara ya kikazi na kuzungumza na wachimbaji katika eneo la Mwakitolyo lililopo Shinyanga Vijijini. Waziri Mavunde alitangaza habari hizo njema kuwa, tayari Shirika la STAMICO limeanza utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais na kwamba eneo limeshapatikana katika Kijiji cha Mawemelu na ujenzi utaanza hivi karibuni. ...

Katibu Mkuu wa Ccm Afanya Mazungumzo na Balozi wa China

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, leo Jumatatu, Desemba 22, 2025, amefanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mheshimiwa Chen Mingjian, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao, wamejadili masuala mbalimbali yenye lengo la kuendelea kuimarisha uhusiano wa kihistoria na urafiki wa kidugu kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), pamoja na uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China.