Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameziagiza idara na taasisi za utafiti na elimu ya juu ziendelee kufanya tafiti za kisayansi ili kutafuta suluhisho za changamoto zenye mwingiliano wa afya ya binadamu, afya ya wanyama, na afya ya mazingira. Ameongeza kuwa idara na taasisi za Serikali zinapaswa kutumia matokeo ya tafiti hizo katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kitaifa. Ametoa maagizo hayo jana (Jumatatu, Novemba 04, 2024) alipofungua Mkutano wa Kitaifa wa Afya Moja katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) Jijini Arusha. Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Taasisi zinazohusika na masuala ya afya ya jamii, wanyama na mazingira zitenge fedha na kuweka katika mipango ya taasisi hizo afua za kuthibiti magonjwa ya kizonotiki, usugu wa vimelea dhidi ya dawa, magonjwa yasiyoambukiza, mabadiliko ya tabia nchi, na usalama wa chakula. “Wizara za kisekta, na Mamlaka za Serikali za Mitaa, andaeni mipango kazi na taratibu za usimamizi kwa ajili ya utekeza...
Marato tv - Sauti ya Jamii