📌 *Dkt. Biteko kuifanya Uyovu kuwa kitovu cha biashara Bukombe* Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amesema kuwa mgombe Urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameiwezesha Kata ya Uyovu kimaendeleo hivyo wananchi hao hawana budi kumpigia kura nyingi Oktoba 29 mwaka huu. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 17, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Uyovu wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. “ Hakuna siku ambayo nilimuomba maendeleo Dkt. Samia kwa ajili ya watu wa Uyovu na Geita akatunyima, ametupa fedha za ujenzi wa barabara nyingi ikiwemo ya kutoka Ushirombo hadi Katoro hata juzi tulimuomba barabara ya Geita kwenda Nzela hadi Sengerema kwa kiwango cha lami yote haya atatusaidia huyu ni mama ni msikivu,” amesema Dkt. Biteko. Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wa Dkt. Samia chini ya CCM kati...
Marato tv - Sauti ya Jamii