Mhandisi Mwandamizi katika Sekta ya Ujenzi, Eng. Magesa Mwita amesema hatua ambayo inachukuliwa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya ujenzi wa shule za mchepua wa Sayansi na ufundi nchi nzima itawezesha kutoa jawabu la tatizo kubwa la ajira kwa vijana nchini. Mhandisi Magesa ametoa kauli hiyo Oktoba 16 mwaka huu 2025 mjini Musoma wakati akihutubia wanafunzi,walimu na wazazi wa shule ya Sekondari ya Morembe katika mahafali ya kidato cha nne ya wanafunzi wa shule hiyo. Amesema Serikali imefanya uwekezaji mkubwa wa shule hizo kwa kila mkoa nchini kama moja ya mkakati wa kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kukabiliana na tatizo la ukisefu wa ajira kwa vijana Kwa sababu hiyo amewapongeza wahitimu katika mahafali hayo, huku akitoa wito kwa wanafunzi wote kuweka mkazo kwa masomo ya mchupua wa Sayansi kwani amesema kufanya hivyo kutawawezesha kufika mbali na kumudu changamoto za kimaisha. "Wanafunzi wote wekeni mkazo kwenye masomo ya Saya...
Marato tv - Sauti ya Jamii