Skip to main content

Posts

Showing posts from August 8, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

MWANA FA ASHUKA CCM KIRUMBA, AAHIDI KUMALIZA KERO YA TAA ZA USIKU

 Na Mashaka Mhando, MWANZA SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, imeahidi kumaliza changamoto ya ukosefu wa taa katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, ili kuwezesha uwanja huo mkongwe kutumika kwa mechi na matamasha nyakati za usiku. Ahadi hiyo nzito imetolewa leo, Agosti 8, 2026, na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma (maarufu Mwana FA), wakati alipofanya ziara maalum ya kukagua miundombinu ya uwanja huo, huku akisisitiza kushirikiana na wadau wa michezo kutatua kero hiyo. Mhe. Mwinjuma amebainisha kuwa dhamira kuu ya Serikali ni kuhakikisha miundombinu yote ya michezo nchini inaboreshwa na kufikia viwango vinavyokidhi mahitaji ya sasa. "Moja ya changamoto kubwa iliyopo hapa Kirumba ni ukosefu wa mfumo wa taa unaowezesha uwanja kutumika kwa ufanisi nyakati za usiku. Hali hii imekuwa ikipunguza fursa za kufanyika kwa baadhi ya shughuli za michezo, hususan mechi na matukio yanayohitaji matumizi ya uwanja wakati wa usiku, naahidi hili nita...

TREASURY REGISTRAR HOLDS TALKS WITH TDB PRESIDENT

 By the OTR Reporter Dar es Salaam. Treasury Registrar Mr Nehemiah Mchechu has held talks with Trade and Development Bank (TDB) President and Managing Director Mr Admassu Tadesse on strengthening the bank’s partnership with Tanzania, with a focus on supporting economic development and unlocking greater value from public investments. The talks, held on Friday, August 7, 2026, at the Office of the Treasury Registrar (OTR) in Dar es Salaam, brought together Mr Mchechu and Mr Tadesse alongside officials from both sides to discuss opportunities for deeper cooperation in investment financing, trade and development. The engagement is of particular significance given that the Government, through the OTR, holds an 8.3 per cent stake in TDB, making Tanzania one of the bank’s shareholders. Mr Mchechu said a stronger partnership with TDB could help expand investment, trade and access to capital for projects with the potential to generate broad economic benefits. He noted that, as a regional de...

MSAJILI WA HAZINA ATETA NA RAIS WA BENKI YA BIASHARA NA MAENDELEO

 Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam.  Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara na Maendeleo (TDB), Bw. Admassu Tadesse, kuhusu namna benki hiyo inavyoweza kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Mazungumzo hayo yana umuhimu wa kipekee kwa Tanzania kwa kuzingatia kwamba Serikali, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, inamiliki asilimia 8.3 ya hisa katika TDB na hivyo kuwa miongoni mwa wanahisa wa benki hiyo ya maendeleo ya kikanda. Mazungumzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi ya Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam yalijikita katika maeneo mbalimbali ya ushirikiano, ikiwemo namna TDB inavyoweza kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Tanzania na kuimarisha ufanisi wa uwekezaji wa Serikali. Bw. Mchechu alisema ushirikiano kati ya Tanzania na TDB ni muhimu katika kuendeleza uwekezaji, biashara na upatikanaji wa mitaji...

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU YA JUMUIYA YA URU SEMINARI

 *ASISITIZA SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA TAASISI ZA DINI KATIKA MAENDELEO YA TAIFA HUSUSANI SEKTA YA AFYA NA ELIMU* Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa Taasisi za Dini ambazo kwa namna ya pekee zimekuwa zikishiriki katika kutoa mchango kwenye sekta za Afya na Elimu hapa nchini. Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Ibada ya Misa Takatifu Maalum ya Wanajumuiya wa Uru Seminari, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kristo Mchungaji Mwema – Tabata Kimanga Jijini Dar es Salaam. Amesema kwa miaka mingi na kwa asilimia kubwa Taasisi za dini zimechangia katika utoaji wa huduma za elimu na afya, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi hizo ili kufanikiwa zaidi katika kulijenga Taifa. Makamu wa Rais amesema Malezi yanayotolewa katika Taasisi za elimu za dini ikiwemo Shule ya Uru Seminari ambayo husisitiza Sala, Kazi na Masomo yanapaswa kutiliwa mkazo katika mal...

RAIS SAMIA AKABIDHI ZAWADI MBALIMBALI WASHIRIKI WA MAONESHO YA KILIMO YA NANE NANE DODOMA

  Matukio mbalimbali katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.

RAIS SAMIA AKABIDHI ZAWADI MBALIMBALI WASHIRIKI WA MAONESHO YA KILIMO YA NANE NANE DODOMA

 Matukio mbalimbali katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Maonesho vya Dkt. John Samuel Malecela, Jijini Dodoma, tarehe 08 Agosti, 2026.

MWANACHAMA WA TBN VERONICA MREMA ATAJWA TUZO YA ISU ELIHLE 2026 - AFRIKA

 Na Mwandishi Wetu Mtanzania Veronica Mrema , mwanachama wa Mtandao wa Mabloga Tanzania , TBN, anayeendesha jukwaa la kidijiti la M24 TANZANIA MEDIA ni miongoni mwa waandishi wa habari sita waliochaguliwa kuendelea na mchakato wa tuzo za ISU Elihle kwa mwaka 2026 Barani Afrika. Veronica ametajwa katika orodha hiyo baada ya wazo lake la habari kuhusu watoto wanaoishi na ugonjwa wa Siko Seli kupitiwa, na kuonekana ni bora. Jopo la majaji wa tuzo hizo limesema kulikuwa na mawazo 155 ambayo walipokea kutoka nchi mbalimbali za Afrika. Hatua ya Veronica kutajwa kwenye tuzo hiyo inaongeza rekodi nzuri katika uandishi wa habari za afya na maendeleo na kuiweka Tanzania katika nafasi ya kuendelea kutoa waandishi wa habari wanaotumia kalamu zao kuibua changamoto za watoto na kuchochea mabadiliko yenye manufaa kwa jamii. Kupitia wazo lake lililochaguliwa Veronica atafanya uchunguzi na kuibua simulizi kuhusu mzigo unaoongezeka wa ugonjwa wa Siko Seli miongoni mwa watoto nchini Tanzania, akia...

WAZAZI WATAKIWA KUWAPELEKA WATOTO MICHEZONI, POLISI YATOA SABABU

 Na Angela Sebastian ;Muleba Wazazi wametakiwa kuwaruhusu watoto na vijana wao kushiriki katika michezo kwani huwajengea Afya bora,kuwapatia ajira na kuwaepusha kuingia katika janga la matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii. Wito huo umetolewa  na Afisa mnadhimu mkoa wa Kagera kamishna msaidizi wa polisi (ACP) Yussuf Daniel wakati akimwakilisha kamanda wa polisi wa mkoa huo Blasius Chatanda katika fainali za Mwijage CUP yaliyofanyika Kamachumu Wilaya ya Muleba mbapo,amemshauri mkurugenzi na mwandaaji wa mashindano ya Paul Mwijage Cup kuanzisha pia timu za vijana chini ya miaka 17  ili kuibua vipaji halisi vinavyopatika Kamachumu. "Mitandao ya kijamii wengi wetu wananchi tunaitumia vibaya,pale tunapoitumia vibaya inaleta athari kubwa kwa kijana mmoja mmoja,kwa wale wa Kamachumu lakini pia kwa jamii yetu yote kwa ujumla hivyo, ni vyema kujiepusha na ombwe hilo ili tubaki salama"amesema Yussufu  Pia amemshauri mkurugenzi wa mashindano hayo kuanzisha timu ya vijana wadog...

CHATANDA: MIKOPO ASILIMIA 10 IMEBADILI MAISHA YA WANANCHI MBALIZI

 NA: MWANDISHI WETU Mpango wa serikali wa kutoa mikopo isiyo na riba ya asilimia kumi kwa wanawake, vijana na wenye mahitaji maalum, imeonyesha kuzaa matunda kwa wananchi wa Mbalizi mkoani Mbeya. Hii ni kutokana wa wanufaika wa mikopo hiyo kuitumia kwa malengo ya kujikwamua kiuchumi na kubadili hali za maisha yao. Matokeo chanya hayo yameonekana katika ziara ya Wajumbe wa Baraza la Utekelezaji la Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Taifa, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mary Chatanda, Agosti 6, 2026. Akiwa katika ziara hiyo, Chatanda ametembelea kikundi cha wauzaji wa nafaka ambacho kimenufaika na mkopo wa shilingi milioni 56. Kikundi hicho kimefanikiwa kurejesha robotatu ya mkopo huo. Kutokana na uaminifu huo, Chatamda ameeleza wakimaliza mkopo huo, wakopeshwe tena kwa kuwa wamefanya vizuri katika marejesho ya mkopo wao. "Mmefanya vizuri kukopa ili mjikwamue kiuchumi, na kwa kuwa mmefanikiwa kurejesha robotatu ya mkopo wenu, nitoe wito kwa uongozi wa Halmashauri kuwako...