Skip to main content

Posts

Showing posts from October 4, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu aanza ziara ya kikazi Temeke,Jijini Dar kwa kishindo

  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 05, 2024 ameanza ziara ya kikazi katika wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam. Katika ziara hiyo Mheshimiwa Majaliwa atakagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuzungumza na wananchi pamoja na watumishi wa umma.

WAZIRI MKUU KUANZA LEO ZIARA YA SIKU MBILI DAR

Katika ziara hiyo inayoanza asubuhi hii October 05 katika halmashauri ya wilaya ya Temeke,mh Waziri mkuu Kassim Majaliwa,atakutana na watumishi,kisha kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo kabla kufanya mkutano wa hadhara eneo la Mbagala rangi Tatu. Kesho ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake,mh Waziri mkuu atafanya ziara kama hiyo wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Gmtv George Marato akutana na mchezaji wa yanga Max Zengeli

Marato na Zengeli wamekutana baada ya kushiriki ibada ya maombi ya Pastor Tony,Millennium Tower's  jijini Dar es Salaam October 04-2024 

Serikali kulipa billioni 16 kuokoa shamba la ushirika mkoani pwani

  Na MWANDISHI WETU Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imekubali yaishe baada ya kuridhia kulipa shilingi bilioni 16 ili kuliokoa shamba la ushirika wa wakulima wadogo wa umwagiliaji Ruvu Chauru, lililopo Mkoa wa Pwani.  Hayo yamebainika wakati Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe  akikagua maendeleo ya chama cha ushirika cha wakulima wa kilimo cha umwagiliaji Ruvu, Chauru Limited 2000, na kuzungumza na wakulima. “Shamba hili litapimwa kwa ushirikiano kati ya wizara na wilaya na mipaka yake itatambuliwa na kuwekwa alama za Tanroad”, amesema Waziri Bashe Bashe amesema kuwa Wizara ya Kilimo italipa fedha hizo zaidi ya shilingi bilioni 16 na kuweka makubaliano maalum na wakulima ili waendelee kutumia shamba hilo.  “Katika kata hii wakulima wanalima hekta 1800, sawa na zaidi ya hekari 2500,hivyo Tume ya Taifa ya Umwagiliaji NIRC itatangaza tenda kwa ajili ya uwekaji wa miundombinu ya umwagiliaji na uzio ili wafugaji wasiingie ndani ya mashamba na wakulima walime kwa uhuru....

Wizara ya Madini,Tume ya madini na Bot yakutana na wadau wa madini

Ikiwa ni mkakati wa kujenga uelewa kwa wadau wa madini kuhusu utekelezaji wa kifungu cha 59 cha Sheria ya Madini Sura 123, leo Oktoba 04, 2024 Wizara ya Madini imeratibu mkutano wa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini uliofanyika jijini Dodoma ambapo elimu kuhusu utekelezaji wa sheria hiyo imetolewa na wataalam kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Viongozi walioshiriki katika mkutano huo ni pamoja na Kamishna Msaidizi – Uendelezaji Migodi, Mhandisi Ally Samaje aliyemwakilisha Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, Meneja wa Masoko ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Lameck Kakulu, Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji wa Madini Tanzania (FEMATA), John Bina, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini kutoka Tume ya Madini, CPA. Venance Kasiki na watendaji wengine kutoka Tume ya Madini. Akizungumza kwa niaba ya Kamishna wa Madini, Dkt. Abdulrahman Mwanga, Kamishna Msaidizi – Uendelezaji Migodi kutok...

Rais Samia amesema lazima uwepo mfumo mzuri wa ulipaji wa kodi nchini

Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amesema ili kufikia lengo la uchumi Jumuishi unaokuwa kwa kasi,unaoimarisha ustawi wa watu kwa kuboresha huduma za Jamii na kupunguza umaskini wa kipato,nchi inapaswa kuwa na mfumo mzuri wa ulipaji na ukusanyaji wa kodi.  Dkt.Samia ameyasema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tume ya Rais ya kutathmini na kushauri kuhusu masuala ya kodi iliyofanyika ikulu ya chamwino. Dkt.Samia amesema kuwa Tume hiyo imeundwa kwa lengo la kufanya tathmini ya mfumo mzima wa kodi,kuimarisha zaidi mfumo huo na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kurahisisha usimamizi wa kodi nchini.  "Licha ya uchumi wa nchi kukua kwa kasi,idadi ya watu kuongezeka na mahitaji ya huduma za Jamii na miundombinu kukua,bado asilimia 60 ya uchumi wa nchi unatokana na sekta isiyo rasmi" alisema Rais Samia na kuongezeka kuwa  "Serikali imedhamiria kujenga mfumo wa kodi unaotenda haki na utakaomuwezesha kila anayestahili kulipa kodi,kulipa kodi stahiki na kutoza kodi zote ...

Biteko kufungua maonesho ya madini Geita

- RC Shigella atembelea Banda la Tume ya Madini  Mwandishi Wetu NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko atazindua Maonesho ya Saba ya Kitaifa ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini Geita yaliyoanza Oktoba 2, kwenye viwanja vya Bombambili mkoani Geita. Akizungumza katika Banda la Tume ya Madini Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigella ambae aliongozana na Afisa Madini Mkazi wa Geita, Samwel Shoo, amesema mwaka huu kuna washiriki zaidi ya 600. Amesema, Maonesho ya mwaka huu yatakua na washiriki kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Congo, Rwanda, Burundi na Kenya. "Ni fursa kwa wachimbaji wadogo, wa kati na wakubwa, watumie maonesho haya kuja kujifunza teknolojia mbali mbali ya sekta ya madini, kuna Banda la Wizara ya Madini na Taasisi zake ikiwemo Tume ya Madini hivyo watanzania wenye nia ya kuwekeza kwenye sekta ya madini watembelee mabanda haya kujifunza na kupata elimu katika mnyororo mzima wa sekta ya madini," amesema Mhe. Shigella. Aidha, amewatak...