Skip to main content

Posts

Showing posts from April 15, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Asilimia 30 ya Zabuni Za Umma: Fursa Adhimu Kwa Vijana na Makundi Maalum

SERIKALI imeendelea kusisitiza utekelezaji wa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 inayotaka taasisi zote za umma kutenga asilimia 30 ya bajeti ya ununuzi kwa ajili ya makundi maalum, yakiwemo vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu, ikiwa ni mkakati wa kukuza uchumi jumuishi nchini. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa PPRA, Bw. Dennis Simba, wakati akiwasilisha mada kuhusu fursa za zabuni za umma kupitia Mfumo wa NeST, katika kongamano la kuadhimisha miaka 104 ya kuzaliwa kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Kongamano hilo lilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma na kufunguliwa Rasmi na Makamu wa Rais, Dkt. Emmanuel Nchimbi. Katika wasilisho lake, Bw. Simba alibainisha kuwa mfumo wa NeST umeboreshwa ili kurahisisha ushiriki wa makundi maalum katika zabuni za umma, huku akihimiza vijana kuchangamkia fursa hizo ili kujijengea uwezo wa kiuchumi. “Sheria hii siyo tu mwongozo wa manunuzi, bali ni chombo muhimu cha kuwawezesha wananchi kiuchumi, hasa makundi maalumu ...

Dkt Mwigulu Awasili Kigoma: Anatarajia Kufungua Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Ziwa Tanganyika

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewasili mkoani Kigoma hii leo, Alhamisi Aprili 16, 2026, ambako anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Ziwa Tanganyika (Lake Tanganyika Business and Investment Forum). Kongamano hilo linawakutanisha viongozi wa Serikali, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchi zinazozunguka ziwa Tanganyika, zikiwemo Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Tanzania ambayo ni mwenyeji wa kongamano hilo lililoanza jana Jumatano, Aprili 15 ambapo litatamatika Jumamosi, Aprili 18, 2026. Akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kigoma, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu amepokelewa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Simon Sirro.

Mabalozi Wastaafu Kuongeza Nguvu katika Kuimarisha Demokrasia ya Nchi

Na Mwandishi wetu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeanza kuweka utaratibu wa kutumia hazina ya maarifa na uzoefu kutoka kwa Mabalozi Wastaafu ili kuimarisha utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kuimarisha diplomasia ya nchi.  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo , amebainisha utaratibu huo leo Aprili 15, 2026, jijini Dar es Salaam wakati anafungua kikao cha mashauriano kati ya uongozi wa Wizara na Mabalozi Wastafu.  "Wizara tumeanzisha utaratibu wa kuwa na vikao vya mara kwa mara na Mabalozi Wastaafu ili kuvuna maarifa na uzoefu wao kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia ili ulete nanufaa katika nyanja mbalimbali kama vile, siasa, ulinzi na usalama, uchumi, biashara, uwekezaji na utalii". Balozi Kombo alisema. Balozi Kombo ametaja mifano ya maeneo ambayo angependa Mabalozi Wastaafu wachangie maarifa na uzoefu walio kuwa nao ili maeneo hayo yaendelee kuwa na manufaa zaidi kwenye nchi. M...

Tanzania Yaunga Mkono Azimio la Mabunge ya Nam-pn Kulipatia Bunge la Kiarabu Hadhi ya Mwangalizi

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Daniel Sillo (Mb) amehutubia Mkutano wa 5 wa Mabunge Wanachama wa Mtandao wa Kibunge wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM-PN) na kueleza kwamba Bunge la Tanzania linaunga mkono Azimio la kulipa Bunge la Kiarabu hadhi ya mwangalizi.  Mhe. Sillo  ameyasema hayo leo, tarehe 15 Aprili 2026 wakati akimuwakilisha Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Mussa Azzan Zungu kwenye Mkutano huo wa 5 wa NAM-PN uliofanyika katika Hoteli ya Hilton Istanbul  Bomonti, jijini Istanbul, nchini Uturuki na aliambatana na Mhe. Elibariki Kingu (Mb). Katika azimio hilo, mabunge wanachama yametambua umuhimu wa msingi wa kuendeleza uhusiano na taasisi nyingine za kimataifa kama sehemu muhimu ya ujenzi wa kitaasisi na uendeshaji wenye ufanisi wa NAM-PN. Aidha, azimio hilo limezingatia maombi rasmi yaliyowasilishwa na Bunge la Kiarabu ya kutaka kuwa na hadhi ya mwangalizi katika mtandao huo. Kwa hatua hii, Bunge la Kiarabu sasa litashiriki vikao na shughuli za ...

Waziri Mavunde Apeleka Kicheko, Kilio Kwa Wachimba Madini

 SERIKALI imetangaza kufuta leseni 40 za uchimbaji wa madini kwa wamiliki walioshindwa kutekeleza masharti ya kisheria, ikisisitiza kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha sekta ya madini inachangia kikamilifu maendeleo ya uchumi wa Taifa. Hatua ya kufuta leseni 40 inaashiria msimamo thabiti wa Serikali wa kuendeleza Sekta ya Madini dhidi ya uzembe na vitendo visivyo halali, huku ikifungua ukurasa mpya wa uwajibikaji na ushindani wa haki katika matumizi ya rasilimali za Taifa. Akizungumza kuhusu uamuzi huo, Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema tayari walishatoa hati za makosa kwa wahusika, lakini bado hawakukidhi matakwa ya sheria, hivyo kulazimika kuchukua hatua ya mwisho ya kufuta leseni hizo kwa mujibu wa sheria. “Kuna wamiliki wa leseni ambao hawaziendelezi kwa wakati, wanahodhi maeneo, hawalipi ada stahiki, na hawatekelezi wajibu wa ushirikishwaji wa Watanzania pamoja na wajibu kwa jamii,” amesema Aidha, amesema kuwa Kuna baadhi ya wamiliki hao wanashindwa hata kuw...

Usambazaji wa mitungi ya gesi ya ruzuku waanza rasmi

📍 *Pangani, Tanga*  Wilaya ya Pangani mkoani Tanga imepiga hatua muhimu katika kuboresha maisha ya wananchi  kupitia mradi wa uuzaji na usambazaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku.  Akizungumza wakati wa hafla ya kutambulisha mradi huo mbele ya katibu tawala wa Wilaya ya Pangani, Bi. Ester Gama, msimamizi wa mradi  kutoka REA, Ndugu Abdulrazack Mkomi ameeleza kuwa lengo kuu la mradi huo ni kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, ambayo yamekuwa yakichangia uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kiafya kwa wananchi, hasa wanawake na watoto. Alifafanua kuwa kupitia mradi huo, mitungi ya gesi ya kilo sita itapatikana kwa bei nafuu ya shilingi 17,500 tu kutokana na ruzuku iliyotolewa, hali itakayowezesha wananchi wengi zaidi kuimudu na kuanza kutumia nishati mbadala iliyo rafiki kwa mazingira.  Aidha, mfumo mzuri wa usambazaji umeandaliwa ili kuhakikisha mitungi hiyo inawafikia walengwa ambao ni wananchi waishio maeneo ya vijijini na mwananchi atat...