Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt, Rhimo Nyansaho (Mb) tarehe 14 Januari, 2026, jijini Dodoma, amezindua Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakurugenzi wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa-SUMAJKT, itakayoongozwa na Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo, aliyeteuliwa hivi karibuni na Waziri wa Ulinzi na JKT. Akizindua Bodi hiyo ya ushauri ya shirika hilo aliyoiteua, Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt Rhimo Nyansaho, amewapongeza wajumbe hao wapya wa bodi hiyo ya SUMAJKT kwa kuteuliwa kwao kuliongoza Shirika hilo na akawaambia ni Imani yake, kuwa Shirika litapiga hatua kubwa zaidi katika kukidhi madhumuni ya kuanzishwa kwake mwaka 1981. Waziri Nyansaho amewaambia Wajumbe hao wapya wa SUMAJKT kuwa hadi sasa shirika hilo limepiga hatua kubwa na nzuri katika miaka ya karibuni ambapo kwa kiasi kikubwa uzalishaji Mali na Malezi ya Vijana, na Shirika limekuwa na miradi mingi yenye tija kwa Taifa na kuleta maendeleo. Waziri wa Ulinzi na JKT akatoa P...
Marato tv - Sauti ya Jamii