**Amuagiza Mkurugenzi Mtendaji TANESCO kumchukulia hatua mtaalam aliyemfokea mteja* 📌 *Ataka Mpango Mahsusi wa Nishati uliosainiwa katika Mkutano wa Mission 300 kupewa kipaumbele* 📌 *PURA, REA, EWURA zang'ara tathmini ya utendaji kazi Taasisi chini ya Wizara ya Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameeleza kutoridhishwa kwake na Kituo cha Huduma kwa wateja cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kusema huduma duni zinasababisha malalamiko kutoka kwa wateja. Dkt. Biteko amesema hayo leo wakati wa Kikao cha Tatu cha Tathmini ya Utendaji Kazi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati katika kipindi cha Oktoba-Desemba 2024 ikiwa ni utaratibu aliouanzisha kwa lengo la wa kujipima katika kila baada ya miezi mitatu ili kuboresha utendaji wa kazi wa Wizara na Taasisi zake. “Pamoja na kazi zote nzuri mnazozifanya lakini eneo ambalo bado hatujafanya vizuri ni utoaji wa huduma kwa wateja, juzi nilitembelea kituo hiki nikawaambia sifurahishwi na utenda...
Marato tv - Sauti ya Jamii