Skip to main content

Posts

Showing posts from February 4, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Utendaji Kazi Kituo Cha Huduma Kwa Wateja Tanesco Wamkwaza Dkt. Biteko

**Amuagiza Mkurugenzi Mtendaji TANESCO kumchukulia hatua mtaalam aliyemfokea mteja* 📌 *Ataka Mpango Mahsusi wa Nishati uliosainiwa katika Mkutano wa Mission 300 kupewa kipaumbele* 📌 *PURA, REA, EWURA zang'ara tathmini ya utendaji kazi Taasisi chini ya Wizara ya Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameeleza kutoridhishwa kwake na Kituo cha Huduma kwa wateja cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kusema huduma duni zinasababisha malalamiko kutoka kwa wateja. Dkt. Biteko amesema hayo leo wakati wa Kikao cha Tatu cha Tathmini ya Utendaji Kazi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati katika kipindi cha Oktoba-Desemba 2024 ikiwa ni utaratibu aliouanzisha kwa lengo la wa kujipima katika kila baada ya miezi mitatu ili kuboresha utendaji wa kazi wa Wizara na Taasisi zake. “Pamoja na kazi zote nzuri mnazozifanya lakini eneo ambalo bado hatujafanya vizuri ni utoaji wa huduma kwa wateja, juzi nilitembelea kituo hiki nikawaambia sifurahishwi na utenda...

Edwin Soko Aeleza Athari Za Kuamua Kusimamisha Misaada Kwa Afrika Kwa Siku 90 na Serikali ya Trump

Anaandika Mwandishi mkongwe Edwin Soko.  Nimeamua kuandika makala hii fupi Kwa kushika kalamu yangu na kuwasilisha uchambuzi wangu mfupi juu ya maamuzi ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kumsimamisha Misaada Kwa siku 90. Serikali ya Rais Donald Trump ilichukua hatua ya kusimamisha misaada kwa nchi za Afrika kwa kipindi cha siku 90, na hii ina athari kubwa kwa sekta mbalimbali, hususan sekta ya afya, elimu, na habari. Misaada kutoka kwa serikali ya Marekani ni muhimu sana kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika nchi nyingi za Afrika, na kusimamishwa kwa misaada hii kutasababisha changamoto kubwa. 1. Athari kwa Sekta ya Afya: Misaada ya Marekani imesaidia sana katika kuboresha huduma za afya Afrika, ikiwemo kupambana na magonjwa kama VVU/UKIMWI, malaria, na kifua kikuu. Kusimamishwa kwa misaada hii kwa kipindi cha siku 90 kutasababisha upungufu wa dawa muhimu, vifaa vya afya, na msaada wa kifedha kwa miradi ya afya inayohusiana na kupambana na magonjwa haya. Hii inaweza kuathiri...

Bodi ya Wadhamini -Tanapa yapongeza Ufanisi wa Zoezi la Kuhama Kwa Hiari Wakazi Wa Nyatwali

Na. Brigitha Kimario - Bunda  Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) walitembelea eneo la Nyatwali lililopo Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara kukagua namna zoezi la uhamaji wa hiari  kwa wakazi wa Tamau, Kariakoo, Nyatwali na Serengeti linavyoendelea. Wakikagua  eneo hilo, leo Februari 04, 2025 baada ya kupata taarifa ya maendeleo ya zoezi la Nyatwali kutoka kwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Stephano Msumi ambaye ni Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Serengeti, CPA. Hadija Ramadhani alishuhudia majengo mbalimbali yameshabomolewa na asilimia kubwa ya wananchi wa Nyatwali  wameshahama na zoezi la ulipaji fidia ya makaburi linaendelea kwa utaratibu mzuri na utulivu. "Ninawapongeza sana kwa kuendesha zoezi hili kwa mafanikio, mmefanya zoezi kwa weledi na kwa muda mfupi. Tumeshuhudia nyumba zimeshavunjwa na zoezi la uhamishaji makaburi linaendelea  bila shaka wengine waje wajifunze kutoka kwenu zoezi kama hili linapojitokeza." ...

Kiwanja Cha Ndege Cha Seronera ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti Kufungwa Kwa Siku Tano

 Mamlaka ya Hifadhi za Taifa(TANAPA)imetangaza kufungwa kwa muda kwa Kiwanja cha ndege cha Seronera Kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara.  Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Afisa uhifadhi mkuu,Kitengo cha Mawasiliano (TANAPA) Catherine Mbena imeeleza kuwa Kiwanja cha ndege Seronera kitafungwa kwa muda wa siku tano kuanzia Februari  nane hadi 12 mwaka huu kwa ajili ya kupisha ukarabati unaoendelea kwenye Kiwanja hicho. Kwa mujibu wa Taarifa hiyo,katika kipindi hicho ndege hazitaruhusiwa kutua au kuruka kwenye kiwanja cha ndege cha Seronera.  Hata hivyo,TANAPA imeuhakikishia Umma hususani Wadau wa utalii kuwa Viwanja vingine sita vya ndege vilivyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa Serengeti vitaendelea kufanya kazi kama kawaida katika kipindi hicho.

Waziri wa Ulinzi na Jkt Apokea Ndege Kwa Ajili ya Oparesheni za Kijeshi,Huku Jwtz Likisema Lipo Tayari Wakati Wowote

 Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa DK. STERGOMENA TAX amepokea ndege ya usafirishaji ya kijeshi iliyotolewa na jeshi la falme za kiarabu kwaajili ya kuimarisha sekta ya ulinzi ndani na nje ya nchi,huku JWTZ likisema lipo tayari kwa lolote na wakati wowote kutekeleza majukumu yake. Dkt TAX amesema ndege hiyo pia itasaidia JWTZ katika oparesheni mbalimbali za kijeshi na kiraia ikiwa dhamira ya Rais na Amiri mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan za kuimarisha jeshi la wananchi la Tanzania ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiusalama. Amesema ujio wa ndege hiyo pamoja na mafunzo ya wataalamu ni matunda yanayotokana na mahusiano mazuri kimataifa yanayofanywa na Rais DK. SAMIA SULUH HASSAN kwani amendelea kuwa mstari wa mbele katika kuimarisha kwa kuhakikisha sera ya mambo ya nje yanatafsiriwa kwa vitendo. Aidha amewataka wataalamu waliopatiwa mafunzo kuhakikisha wanafanya kazi kwa kujiamini kwani serikali ya awamu ya sita inathamini mchango wa jeshi na wakati wote itaendelea k...

Samia: Dunia imetambua Jitihada Za Tanzania Katika Sekta ya Afya

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa Tuzo Maalum ya Kimataifa ya The Global Goalkeeper Award inathibitisha kuwa dunia imetambua juhudi za Tanzania katika kuboresha huduma za afya, hususan kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano. Rais Dkt. Samia amesema kuwa serikali anayoiongoza imeweka mipango madhubuti na kuongeza jitihada zaidi ili kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030, Tanzania inavuka lengo la kimataifa la kupunguza vifo vya akina mama, watoto wachanga na watoto chini ya miaka mitano. Mhe. Rais Dkt. Samia aliyasema hayo leo Jumanne, tarehe 4 Februari 2025, alipowahutubia waandishi wa habari mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma, akitokea jijini Dar es Salaam, ambako alipokea tuzo hiyo maalum ya kimataifa. “Tuzo hii ina maana kubwa sana. Dunia imetambua jitihada zetu katika kuboresha huduma za afya, hasa afya ya mama na mtoto. Miaka minne iliyopita,...

Utendaji kazi na bidii vyampandisha cheo askari mmoja wa Jeshi la Polisi Mara

  Na Ada Ouko, Mara. KAMANDA wa jeshi la polisi Mkoa wa Mara Kamishina Msaidizi Mwandamizi (SACP) Pius Lutumo amemvisha cheo cha sajenti polisi kata wa kata ya Ikoma wilayani Serengeti Koplo Emmanuel Kisiri. Wadhifa huo umetolewa baada ya kuonyesha bidii na jitihada kubwa katika utendaji wake wa kazi Koplo Kisiri ambaye ni polisi wa kata hiyo amepewa wadhfa huo leo february 4 mwaka huu 2025 katika viwanja vya kikosi cha kutuliza ghasia Kamnyonge Manispaa ya Musoma mkoani hapa. Aidha baada ya kumvisha cheo hicho kamanda Lutumo amesema kuwa askari huyo anapaswa kuwa mfano wa kuigwa, na kwamba ushirikiano wake na kujiweka karibu zaidi na jamii anayoihudumia sanjari na wadau mbalimbali ndio umempelekea kupata cheo hicho. "Kutokana na jitihada alizozionyesha Koplo Emmanuel Kisiri ni dhahiri kuwa ana uwezo wa kuongoza hivyo anastahili kutunukiwa cheo cha sajenti" amesema Kamanda Lutumo. Mwisho.