Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, ameongoza uzinduzi wa Ripoti ya Ufuatiliaji wa Fedha zinazoingia katika nchi kutoka kwa Watanzania wanaoishi ughaibuni (Cross-border Remittance Diagnostic), katika ofisi za BoT jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwenye uzinduzi wa Ripoti hiyo, Gavana Tutuba amelishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) kwa msaada wake wa kiufundi katika kufanya utafiti huo ambao una mchango mkubwa katika kustawisha sekta ya fedha nchini. “Nianze kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa UNCDF kwa msaada wa kiufundi walioutoa ambao ulisaidia katika katika utafiti huu, ambao ripoti yake inazinduliwa leo. Pia, ninashukuru sana kwa wadau wote wa sekta ya fedha walioshiriki katika utafiti huu zikiwemo wizara na mashirika ya umma, mabenki, watoa huduma za mitandao ya simu, watoa huduma za malipo kwa niia kielektroniki, na taasisi zinazotoa huduma ndogo za fedha,” amesema Gavana Tutuba. Aidha, amesisitiza kuwa fe...
Marato tv - Sauti ya Jamii