*Kitakuwa na uwezo wa kuchenjua tani 500 kwa Saa 24* *Kuzalisha Ajira 350 kwa Watanzania* *Ukarabati kuchukua Miezi Miwili* *Chunya* Septemba 2024, jina la Bilionea Aidan Andrea Msigwa lilitikisa Sekta ya Madini kama radi katikati ya jua kali kwa kuuza kilo 111.82 za dhahabu. Alivuna zaidi ya shilingi bilioni 20.11 kwa mkupuo mmoja hatua iliyotikisa si tu wadau wa madini, bali iliwaamsha Watanzania wengi hadi kuvuka mipaka ya nchi. Aidan hakutajwa tu kama gwiji wa madini, bali aliwekwa rasmi kwenye meza ya mabadiliko ya kiuchumi ndani na nje ya Tanzania. Baada ya kuvuna mabilioni kutokana na kuuza dhahabu hiyo Aidan hakukimbilia anasa bali alichagua kuwekeza kwa watu baada ya kutumia kiasi kikubwa cha fedha kuinunua Kampuni ya SUNSHINE Group iliyoko Matundasi Chunya iliyokuwa ikimilikiwa na wawekezaji kutoka China. Kwa sasa yupo mbioni kwa kushirikiana na wawekezaji wengine wa China kukifufua kiwanda hicho kikubwa cha kuchenjua dhahabu kilichokuwa kimesimamisha shughuli zake...
Marato tv - Sauti ya Jamii