Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga Elimu ni gharama. Wahenga wakaweka wazi ukweli huu kwa kusema "Ikiwa unaona elimu ni ghali, basi jaribu ujinga." Ni ukweli ulio dhahiri kuwa gharama za kupata elimu ziko juu, ndiyo maana serikali ikachukua jukumu la kuja na kutekeleza kwa vitendo Sera ya Elimumsingi Bila Ada kuanzia Elimu ya Awali hadi Kidato cha Sita. Hili limefanyika kwa lengo la kuwapunguzia wazazi na walezi mzigo mkubwa wa gharama za kugharamia elimu za watoto na ndugu zao. Serikali sasa inatoa Ruzuku ya Uendeshaji (Capitation Grants) kwa shule zake zote za msingi na sekondari ili kufanikisha shughuli za taaluma, utawala, mitihani, michezo, ukarabati na shughuli nyinginezo ndogondogo katika ngazi ya shule. Kwa upande wa elimu ya kati na ya juu, serikali inatoa mikopo kwa wanafunzi kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ili waweze kumudu gharama za elimu na hatimaye waweze kutimiza ndoto zao za kupata elimu ya juu na hatimaye waweze kujiajiri au kuajir...
Marato tv - Sauti ya Jamii