Skip to main content

Posts

Showing posts from October 26, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Jeshi la polisi lajivua kudhibiti uharamia pamoja na kupunguza uvuvi haramu ziwa Victoria

Na Dawati la Habari Polisi Mwanza Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na wadau wa uvuvi limefanikiwa kudhibiti uhalifu ukiwemo uharamia uliokuwa ukitendaka ndani ya ziwa viktoria kwa kufanya doria, misako na operesheni mbalimbali zilizofanikisha kukamata watuhumiwa , mali za wizi pamoja na zana haramu za uvuvi. Mafanikio hayo yamebainishwa Oktoba 25, 2024  wilayani Busega mkoani Simiyu wakati wa kikao kazi cha Saba cha Makamanda wa Polisi mikoa ya kanda ya ziwa na wadau wa uvuvi kutoka mikoa ya Mwanza, Geita, Simiyu, Tarime Rorya, Kagera na Mara kwa lengo la kujadili usalama ndani ya ziwa viktoria. Akitoa taarifa ya Utekelezaji wa mikakati na maazimio ya kikao kilichopita, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafugwa amesema zaidi ya watuhumiwa 10,000 pamoja na zana haramu za uvuvi zikiwemo zaidi ya nyavu haramu 10,000 zilizokuwa zikitumika kuharibu mazao ya uvuvi zimekamatwa katika kipindi cha miezi sita iliyopita.  Kwa upande wake,Mku...

Rais Samia apongezwa kwa kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia sekondari ya capri-point

Uongozi wa shule ya sekondari ya Capri-point wilayani Nyamagana mkoani mwanza umeishukuru kwa dhati serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mazingira ya kujifunza na kufundishia.  Mkuu wa shule ya sekondari Capri-Point Thomas Mboya amesema kuwa mazingira ya utoaji wa elimu yamekuwa rafiki baada ya kutatuliwa kwa changamoto zilizokuwa zinaikabili shule hiyo.  Uhaba wa vyumba vya madarasa ni miongoni mwa changamoto zilizotatuliwa kwa kuongezwa kwa vyumba 14 vya madarasa vikiwemo 12 vya ghorofa pamoja na vyumba viwili vya kawaida.  Shule hiyo pia imeondokana na uhaba wa na Dawati baada ya serikali kuipatia viti na meza 640. Akizungumza katika mahafali ya 15 ya kidato cha nne,Mboya amesema kuwa vitabu vya masomo ya sayansi na Hisabati si tatizo baada ya kupokea vitabu 3,300 kutoka serikalini huku idadi ya walimu ikiongezeka Hadi kufikia walimu 32. Aidha ameishukuru serikali kwa kuendelea na utekelezaji wa Sera ya elim...

Waziri mkuu amesema mapambano dhidi ya rushwa nchini si la Takukuru pekee

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa mapambano dhidi ya rushwa si jukumu la TAKUKURU pekee bali kila Mtanzania anapaswa kushiriki kikamilifu kusimamia maadili na kupinga vitendo vya rushwa. Amesema kuwa rushwa inaweza kusababisha kutofikiwa kwa jukumu la Serikali la kuleta ustawi wa wananchi linalotamkwa katika Ibara ya 8(1)[b] ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amesema hayo leo (Jumamosi, Oktoba 26, 2024) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla ya ufungaji wa mafunzo ya awali ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU), yaliyofanyika kwenye Shule ya Polisi Tanzania, Moshi mkoani Kilimanjaro. “hili ni jukumu la kila Mtanzania na wadau wote muhimu hapa nchini, rushwa ni adui wa haki na maendeleo katika jamii, Vitendo vya rushwa rushwa vinasababisha uchepushaji wa rasilimali kutoka kwenye matumizi sahihi na kuathiri haki za kiraia. Katika utumishi wa umma, rushwa inavuruga ushindani wenye usawa na inaathiri rasilimaliwatu y...