Skip to main content

Posts

Showing posts from December 20, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri Mkuu akagua Maendeleo ya Mradi wa Maji Kisesa Mwanza

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Desemba 21, 2024 amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa tenki la kuhifadhi maji la Kisesa, mkoani Mwanza ikiwa ni Mpango wa muda wa kati wa kuboresha huduma ya maji Mwanza ambao unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.54. Mradi huo ambao unafadhiliwa na Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (France Development Agency) hadi kukamilika kwake na mpaka sasa umefikia asilimia 93 na unatarajiwa kuhudumia wananchi 75,000 wa maeneo ya Kisesa Bujora, Igudija na swhemu za jirani. Akizungumza na wananchi wa eneo la Kisesa baada ya kukagua mradi huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi mikubwa inayowagusa wananchi moja kwa moja kwenye sekta za elimu, afya, maji, kilimo, uvuvi na barabara. Kwa Upande wake, Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema wizara hiyo itaendelea kusimamia maagizo ya Rais ...

Serikali imeweka Mkakati wa Kupunguza Kesi za Migogoro ya Ardhi

   Na Ada Ouko,Musoma. MRATIBU wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Rais Dkt, Mama Samia Legal Aid Mkoani Mara amesema Serikali imeanzisha mchakato wa kupunguza kesi zinazotokana na migogoro ya ardhi Mahakamani. Buliro amesema hayo hivi karibuni , wakati akitoa elimu ya sheria mbalimbali ikwa ni sheria za ardhi, mirathi, unyanyasaji wa kijinsia kwa wakazi wa mtaa wa Mtakuja "A" kata ya Mwisenge Manispaa ya Musoma "tayari tumepewa maelekezo na wizara ya katiba na sheria tufanye uchunguzi ili kubaini tatizo lakini suala la uhaba wa mwenyekiti pia laweza kuchangia na njia pekee ya kupunguza mashauri ya ardhi ni kuongeza wenyeviti wa mabaraza, walau kila wilaya awepo mwenyekiti mmoja"amesema. Wakili wa kujitegemea kutoka chama cha mawakili Tanganyika Emmanuel Werema alisema mwenyekiti mmoja wa mabaraza ya ardhi anahudumia mashauri 2000 endapo akipatwa na changamoto ya kiafya au kifamilia kesi itasogezwa miezi ya mbele. Aidha alisema mwenyekiti huyo anatoa huduma katika m...

Waziri Mkuu kukagua ujenzi wa mradi wa maji Bujora - Magu

  WAZIRI MKUU KUKAGUA UJENZI WA MRADI WA MAJI BUJORA-MAGU.  Kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa tenki kubwa la maji unaokaguliwa leo Desemba 21, 2024 utawezesha kupokea maji kutoka ziwa Victoria na kutawezesha kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa kata ya Bujora,Bukandwe na Kisesa pamoja na vijiji jirani vya wilaya ya Ilemela.

Waziri Mkuu amesema Sekta ya Utalii ni Nguzo muhimu kwa uchumi wa Taifa.

  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itendelea kubuni mikakati ya kuimarisha sekta ya Maliasili na Utalii kwa kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu kwa uchumi wa Taifa. Amesema hayo jana (Ijumaa, Desemba 20, 2024) wakati alipozindua Tuzo za Uhifadhi na Utalii katika Ukumbi wa Hoteli ya Mt. Meru jijini Arusha. Tuzo hizo zinalengo la kuchochea ushindani kati ya wadau wa sekta ya maliasili na utalii nchini. Amesema kuwa Sekta ya maliasili na utalii ni chanzo kikubwa cha mapato ya Taifa kwa kuwa inahusisha shughuli nyingi za kiuchumi. “Sekta hii peke yake inachangia asilimia 21.5 katika pato ghafi la Taifa ambapo asilimia 17.2 ni utalii, asilimia 4.3 ni misitu na nyuki”. Aidha, amesema kuwa Sekta hiyo inachangia asilimia 30.9 ya mapato ya fedha za kigeni ambapo asilimia 25 yanatokana na utalii na asilimia 5.9 ni misitu na nyuki. Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa juhudi za dhati na maono makubwa ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuiendeleza Sekta ya ...

Serikali imeweka Mkakati wa Kupunguza Kesi za Migogoro ya Ardhi

 Na Ada Ouko,Musoma. MRATIBU wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Rais Dkt, Mama Samia Legal Aid Mkoani Mara amesema Serikali imeanzisha mchakato wa kupunguza kesi zinazotokana na migogoro ya ardhi Mahakamani. Buliro amesema hayo hivi karibuni , wakati akitoa elimu ya sheria mbalimbali ikwa ni sheria za ardhi, mirathi, unyanyasaji wa kijinsia kwa wakazi wa mtaa wa Mtakuja "A" kata ya Mwisenge Manispaa ya Musoma "tayari tumepewa maelekezo na wizara ya katiba na sheria tufanye uchunguzi ili kubaini tatizo lakini suala la uhaba wa mwenyekiti pia laweza kuchangia na njia pekee ya kupunguza mashauri ya ardhi ni kuongeza wenyeviti wa mabaraza, walau kila wilaya awepo mwenyekiti mmoja"amesema. Wakili wa kujitegemea kutoka chama cha mawakili Tanganyika Emmanuel Werema alisema mwenyekiti mmoja wa mabaraza ya ardhi anahudumia mashauri 2000 endapo akipatwa na changamoto ya kiafya au kifamilia kesi itasogezwa miezi ya mbele. Aidha alisema mwenyekiti huyo anatoa huduma katika ma...