Skip to main content

Posts

Showing posts from May 8, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania na Canada kuimarisha uhusiano kwenye utafiti wa Madini

■ Waziri Mavunde aeleza fursa zilizopo kwenye utafiti, ■ Balozi Burns abainisha utayari wa Makampuni ya Canada kuwekeza nchini Tanzania, ▪️Canada yaonesha utayari wa kusaidia teknolojia kwa wachimbaji wadogo  ■ *Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais yaweka Mazingira wezeshi kwa wawekezaji  nchini. *Dodoma* Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Canada nchini Tanzania, *Mheshimiwa Emily Burns* katika ofisi ndogo za Wizara zilizopo katika jengo la Tume ya Madini, Kilimani Jijini Dodoma. Katika mazungumzo hayo, Waziri Mavunde alibainisha kuwa moja ya kipaumbele kikuu cha sekta ya madini ni utafiti ambao utapelekea kutambua aina na kiwango cha rasilimali madini tulizobarikiwa nchini kwetu na kuvutia uwekezaji. "Tunafamu kuwa Nchi yetu tumeweza kufanya utafiti wa kina wa kurusha ndege kwa asilimia 16 tu. Hivyo, tuna uhitaji mkubwa wa kupata uwekezaji zaidi katika eneo hili ili kuongeza mchango wa sekta ya madini kweny...

Baraza la Wafanyakazi ni nguzo ya Ushirikishwaji wa Watu,Mhe.Millya

Imeelezwa   kuwa   Mikutano   ya   Mabaraza   ya   Wafanyakazi   ni majukwaa   muhimu   ya   kuwashirikisha   watumishi   moja   kwa   moja katika mipango ya Serikali ili kupata mawazo mapya na umiliki wa pamoja wa mipango hiyo kwa lengo la kutekelezwa kwa ufanisi na bila manung’uniko.  Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Afrika   Mashariki  (EAC),   Mhe.  James   Millya   wakati  anafungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma Mei 08, 2026. Mhe. Millya alisema kitendo cha Baraza hilo kupitia makadirio ya bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027 kitawapa watumishi fursa ya kupitia maeneo muhimu ya vipaumbele vilivyowekwa na kuboresha mikakati   ya   utekelezaji  ...

Dkt. Mwigulu Aagiza Itafutwe Suluhu ya Kudumu Daraja la Magole–Dumila

  _▪️Ateta na WanaGairo, asisitiza kuitunza amani_ WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya ukaguzi wa daraja la Magole lililopo Dumila katika Mto Mkundi wilayani Kilosa na kuagiza uongozi wa TANROADS utafute suluhu ya kudumu ya changamoto inayolikabili daraja hilo ya kujaa maji na mchanga kila mwaka. Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Mei 8, 2026) wakati akizungumza na wananchi waliofika darajani hapo kumsikiliza na akamtaka Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro ashirikiane na wataalamu wengine kuandaa utaratibu wa kuwaruhusu wananchi kuchimba mchanga katika eneo hilo kwa kuzingatia maelekezo ya kitaalamu, ili kusaidia kupunguza mzigo wa gharama za Serikali na wakati huohuo kulinda miundombinu ya daraja hilo. “Meneja wa TANROADS na wenzako wote ratibuni eneo ambalo tunahangaika kutoa mchanga na hatuna bajeti, wananchi muwaruhusu watoe mchanga huo kwa utaratibu wa kitaalamu,” amesisitiza Waziri Mkuu. Akitoa taarifa kuhusu hali ya eneo hilo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Mal...

Wizara ya Viwanda na Biashara Yaahidi Kuendelea Kukuza Ubunifu na Ujasiriamali Kwa Vijana

Na MATUKIO DAIMA APP MOROGORO  Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imeahidi kuendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha vijana nchini kukuza vipaji vyao vya ubunifu pamoja na shughuli za ujasiriamali, hatua inayolenga kuongeza ajira, kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na kuchochea maendeleo ya taifa kwa ujumla. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Aristides Mbwasi, amesema hayo wakati alipomwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Judith Kapinga, katika hafla ya kufunga maadhimisho ya Siku ya Mzumbe sambamba na Kambi ya Ujasiriamali iliyofanyika katika Chuo Kikuu Mzumbe.  Mbwasi amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na vijana katika kukuza uchumi kupitia bunifu mbalimbali wanazoziibua kila siku, hivyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za elimu ya juu pamoja na wadau wengine wa maendeleo ili kuhakikisha ubunifu huo unakuwa na tija kwa jamii na taifa. Amesema kuwa katika kipindi hiki ambacho dunia imejaa ushinda...

Wizara ya Fedha Yakutanisha Serikali na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Kuimarisha Maendeleo.

Na. Mwandishi wetu, WF, Dodoma Wizara ya Fedha imebainisha kuwa itaendelea kujenga uelewa, kubadilishana uzoefu na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali nchini ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kijamii unakuwa na ufanisi mkubwa. Hayo yalibainishwa na Kaimu Kamishna Msaidizi, Idara ya Fedha za Nje, Wizara ya Fedha, Bw. John Kuchaka, wakati akifungua warsha iliyowakutanisha Serikali na wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkandarasi, jijini Dodoma. Alisema jitihada za Serikali ya Tanzania zimekuwa zikilenga kuhakikisha kuwa maendeleo ya wananchi yanapatikana kwa njia jumuishi na endelevu ambapo mchango wa mashirika hayo ni muhimu katika kufikisha huduma kwa jamii na kuunga mkono juhudi za Serikali kwenye sekta mbalimbali. ‘‘Kupitia warsha hii mafunzo yatatolewa kuhusu masuala muhimu ikiwemo mwongozo wa kufuata taratibu za kifedha kwa wadau wasio wa kiserikali, mwongozo wa bajeti ya Serik...

REA kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia majiko banifu Mkoani Mwanza*

  📍 *Mwanza.* Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Envotec Services Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia REA za kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi, kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira pamoja na kuhifadhi mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda, ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia miradi mbalimbali ya nishati yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku. Amesema mradi huo ni muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwani utasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa pamoja na kusaidia kulinda af...

Wanafunzi Funguni Sekondari Wajifunza Ujasiriamali Kwa Vitendo

NA: MWANDISHI WETU, PANGANI. Utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu unaozingatia umahiri kwa wanafunzi unaendelea kutekelezwa nchi nzima katika kuhakikisha nchi inazalisha wahitimu wenye uwezo wa kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa. Katika Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga, Mei 8, 2026, wanafunzi wa kidato cha pili wa shule hiyo, katika somo la Biashara (Business Studies), wameweza kupika vitafunwa mbalimbali kama chapati, maandazi, sambusa na vitumbua ikiwa ni sehemu ya ujifunzaji kwa vitendo wa uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zilizo katika mazingira yao (local production). Mwalimu wa somo la Biashara wa shule hiyo, Shija Clement amesema baada ya ujifunzaji wa nadharia wa Mada ya Uzalishaji (Production), wanafunzi wanapaswa kuweka ujifunzaji huo kwa vitendo ili kuwajenga katika umahiri na kujitegemea hata baada ya kuhitimu masomo yao ili pia waweze kujiajiri wenyewe na kuanzisha biashara zao. "Wanafunzi wanapaswa kuwa na ujuzi fulani wanapohitimu masomo...

Rais Samia Anyanyua Mkono Kuomba Ruhusa ya Kuzungumza Katika Kikao Cha Shina

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mjumbe wa Shina namba 1 CCM Chamwino akishiriki kikao cha kawaida kilichoitishwa na Balozi wa Shina hilo Bi. Paulina Mkasanga, Chamwino mkoani Dodoma tarehe 8 Mei, 2026.