Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari akiongozana na baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametembelea Kiwanda cha kuchakata gesi asilia cha Madimba na Vitalu vya gesi asilia vilivyoko Msimbati Mkoani Mtwara, tarehe 21 Agosti, 2025. Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa ziara hiyo itawaongezea maarifa Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Upekuzi wa Mikataba na utoaji wa Ushauri kwenye Miradi mikubwa ukiwemo mradi huo mkubwa wa gesi na mafuta. *"Tunapoona mradi huu maana yake ni kwamba kuna mikataba ilitangulia mwanzo mikataba ambayo iliandikwa na kupekuliwa vizuri na vihatarishi vyote vikawekwa vizuri na maslahi ya Taifa yakazingatiwa vizuri."* Alisema Mwanasheria Mkuu wa Serikali Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa ziara hiyo ni sehemu ya mafunzo kwa Wataalamu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, mafunzo ambayo yatawasaidia kuwaongezea uwezo katika masuala ya kiufundi kuhusiana n...
Marato tv - Sauti ya Jamii