Kampuni ya The Wheel Imefungua Kituo Kinachotumia Teknolojia ya Akili Bandia Kutengeneza Magari Dodoma
Na Mwandishi Wetu-Dodoma SEKTA ya matengenezo ya magari inakaribia kushuhudia mapinduzi makubwa baada ya kampuni ya THE WHEEL kuzindua teknolojia mpya ya kisasa inayolenga kuboresha utendaji wa mafundi na kuongeza ufanisi wa kazi zao. Teknolojia hiyo, inayotumia akili bandia (AI) na mifumo ya uchambuzi wa data, inatarajiwa kubadilisha jinsi matatizo ya magari yanavyogunduliwa na kutatuliwa, hivyo kuokoa muda na kuongeza usalama kazini. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi msemaji wa kampuni ya The Wheel Amesema wamefungua kituo Cha utoaji huduma za urekebishaji wa haraka na utunzaji wa magari jijini Dodoma na wamefurahi kupanua huduma hadi Dodoma ambapo lengo ni kuboresha uzoefu wa Uendeshaji Kwa wateja wao huku kituo hicho Ikiwa ni kituo cha saba Cha kutoa huduma nchini Tanzania. Chris Mendoza, ameeleza kuwa teknolojia hii itawapa mafundi uwezo wa kugundua hitilafu kwa haraka zaidi, kupunguza muda wa matengenezo, na kuhakikisha magari yanarejeshwa kwa wateja katika h...