Skip to main content

Posts

Showing posts from July 22, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mhandisi Maryprisca Mahundi: Usalama wa Mtandao Ni Muhimu Kwa Taifa

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amesema suala la usalama wa kimtandao ni muhimu ili kuhakikisha upatikanaji wa taarifa, huduma na bidhaa za mtandaoni ni salama na hazimuathiri mwananchi na Taifa kwa ujumla. Akizungumza wakati wa ziara yake makao makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) tarehe 18 Julai, 2024 Mhandisi Mahundi ameishukuru timu zima ya TCRA kwa umahiri mkubwa katika usimamizi wa sekta hasa katika eneo la usalama mtandao. Amesema, umahiri wa TCRA kunaifanya Wizara kuonekana inawajibika na kuendelea kulipa Taifa heshima huko duniani ambapo mpaka sasa tupo katika nafasi nzuri kimataifa katika masuala ya usalama mtandao. Aidha, ametoa rai kwa TCRA kuendelea kukimbizana na mabadiliko ya teknolojia kwa wataalam kujifunza na kuongeza ujuzi mara kwa mara ili kuweza kukabiliana na wahalifu wa mtandaoni wanaoenda sambamba na kasi ya ukuaji wa teknolojia kwa kubuni mbinu mpya za kufanya uhalifu. Mhandisi Mahund...

Balozi Shelukindo Afungua Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano JPC Baina ya Tanzania na Comoro

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amefungua Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro katika Ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 22-24 Julai 2024. Akizungumza katika mkutano huo wa kihistoria, Balozi Shelukindo ameelezea kuridhishwa kwake na ukuaji wa mzunguko wa biashara kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro ambao umeongezeka kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. “Mzunguko wa biashara kati ya Tanzania na Visiwa vya Comoro umeongezeka kwa kiasi kikubwa katika miaka mitatu iliyopita kutoka Dola za Marekani milioni 6.75 mwaka 2021 hadi Dola milioni 54.67 mwaka 2023”, alisema Balozi Shelukindo. Balozi Shelukindo amesema ukuaji huo wa biashara ni mafanikio makubwa na kusisitiza kuwa bado kuna haja kwa nchi hizo mbili kuongeza uwigo wa ushirikiano wa kiuchumi kwa kutumia fursa zilizopo kwa tija ya pande zote mbili. Amesem...

Biteko Amshukuru Rais Samia Kwa Kupeleka Miradi ya Maendeleo Bukombe

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Mhe. Dkt. Doto Biteko amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa heshima kubwa aliyowapa Watu wa Bukombe kwa kuwaletea Maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesema hayo wakati akihutubia mkutano wa wa hadhara katika Uwanja wa Lyambamgongo Center iliyopo Kata ya Lyambamgongo, Jimbo la Bukombe mkoani Geita. “ Nataka niwambieni mambo mazuri yanakuja, Mama Samia amesema anataka aione Bukombe mpya na mimi nawahakikishieni itabadilika Lyambamgongo haikuwa hivi na ninyi ni mashahidi lakini Rais wetu ametuletea huduma mbalimbali za maendeleo na leo tumepata barabara ya kutoka Lyambamgongo hadi Ifunde, Ishoro, Nyamakungu, hatukuwa na Zahanati leo tumepata Zahanati na Nishati ya umeme wa uhakika mambo mazuri zaidi yanakuja na Bukombe itabadilika”. amesisitiza Dkt. Biteko. Dkt. Doto Biteko amewataka wananchi wa Kijiji cha Lyambamgongo na Jimbo la Bukombe kwa ujumla kujiandaa kwa ajili ya Uchaguzi wa Seri...

Naima Minga Ajitosa Kwa Mara ya Tatu Kuwania Nafasi Ya Naibu Meya Musoma

Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Musoma mjini, leo kimemkabidhi fomu ya kugombea nafasi ya Naibu Meya katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma diwani wa viti maalum katika halmashauri hiyo Mhe. Naima Minga. Fomu hiyo ya CCM imetolewa leo Julai 22-2024 na katibu wa CCM  Musoma mjini  ndugu Barhan  Ruta na endapo atapitishwa na vikao vya chama, vitamwezesha Mhe.Naima kushika nafasi hiyo kwa vipindi  vitatu mfululizo. Mhe.Naima ambaye amekuwa mwanachama wa kwanza kuchukua fomu hiyo leo,amekuwa na mvuto mkubwa wa kuendelea kushika nafasi hiyo kutokana na utendaji wake wa kuridhisha hasa baada ya kuwa kiungo kati ya hamashauri na wananchi pamoja na kusimamia vyema utekelezaji wa ilani ya CCM.  Katika tukio hilo pia limeshuhudiwa na katibu wa UWT wilaya ya Musoma mjini Bi Angel Simwanza, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa azimio la UWT  la kuwapa nafasi za uongozi wanawake pale wanapojitokeza. Uchaguzi wa mgombea wa Naibu Meya anayetokana na CCM unatarajiwa kufan...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

Waziri Mkuu Awataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kusimamia Miradi ya Maendeleo

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya wasimamie miradi yote ya maendeleo kwenye mikoa na wilaya zao na kuhakikisha inakamilishwa ili ianze kutoa huduma kwa wananchi. “Kwenye eneo la usimamizi wa miradi, Wakuu wa Mikoa hakikisheni mnazo taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo; hii ni fursa yenu ya kujua benki tuliyonayo ya utekelezaji wa miradi yote ya tangu mwaka 2021. Angalieni ni miradi gani imepata fedha, na mjiridhishe kama imekamilika au la, na kama bado haijakamilika, fuatilieni ni kwa nini haijakamilika.” Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumatatu, Julai 14, 2024) wakati akizungumza na Kamati za Usalama za Mikoa na Wilaya Pamoja na viongozi wa CCM wa Mikoa kwenye kikao kazi alichokiendesha kwa njia ya mitandao (video conference) kutokea ofisi ndogo ya Waziri Mkuu iliyoko Magogoni, jijini Dar es Salaam.  Waziri Mkuu amesema miradi inayojengwa kwa fedha za Serikali kwenye Halmashauri na Manispaa ni mingi hivyo amesisitiza ikamilishwe kwa asilimia 90 i...

Kadi Za Mpiga Kura Zilizotolewa Mwaka 2015 na 2020 Kutumika Kwenye Uchaguzi

Kadi za mpiga kura zilizotolewa mwaka 2015 na 2020 ni halali na zitaendelea kutumika kwenye chaguzi kuu zijazo bila kujali mabadiliko ya jina la Tume ya Uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Akizungumza wakati wa ziara aliyoifanya ya kukagua vituo vya kuandikishia wapiga kura leo tarehe 22 Julai, 2024 katika Halmashuari ya Wilaya ya Kasulu, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhan amesema wapiga kura wenye kadi hizo hawahusiki na zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga Kura. “Naomba nitoe wito kwa wale ambao kadi zao ni zile zenye jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi na wanadhania kuwa kubadilika kwa jina la Tume kunasababisha kubadili kadi watambue kuwa kadi zao ni halali kwa mujibu wa kifungu cha 168 cha Sheria ya Uchaguzia wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024,” amesema.  Mkurugenzi huyo wa uchaguzi ambaye kwenye ziara yake aliambatana na Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Kasulu Vijin...