Skip to main content

Posts

Showing posts from December 1, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CBE kujenga kampasi mpya Kilimanjaro

Na Mwandishi Wetu CHUO cha Elimu ya Biashara (CBE),kimesema kimeendelea kufanya vizuri kitaaluma ambapo utafiti uliofanyika mwaka jana ulikiweka kwenye nafsi ya nane kati ya vyuo 47 vya elimu ya juu. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Edda Lwoga, wakati wa kongamano la kitaaluma lililofanyika chuoni hapo. Alisema chuo hicho kikongwe kimetimiza miaka 60 ya kubobea kwenye kufundisha biashara, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA na kwa muda wote wa uhai wake kimemudu kuzalisha idadi kubwa ya wataalamu wa kada mbalimbali. Alisema kwa sasa chuo hicho kina kampasi nne za  Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza na Mbeya na mwakani kinatarajia kujenga kampasi yake nyingine mkoani Kilimanjaro kutimiza ahadi iliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa kampeni zake. Alisema katika kudhihirisha ubora wake utafiti uliofanyika mwaka jana ulionyesha chuo hicho kushika nafasi ya nane kati ya vyuo 47 vya elimu ya juu nchini na kwamba mafanikio hayo yamewezes...

Rais Samia Kulihutubia Taifa Kupitia Wazee wa Dar es Saalam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan  anatarajia kuzungumza na wazee wa Dar Es Salaam kesho Desemba 2, 2025 baada ya mikoa huo kuendelea kurejea katika hali yake ya amani. Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa huo Albert John Chalamila wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Disemba 01, 2025 ambapo amesema tukio hilo litafanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa JNICC kuanzia saa tano asubuhi. Ameongeza kuwa Dkt. Samia pia atatumia nafasi hiyo kulihutubia taifa ambapo ataambataana na viongozi wa serikali pamoja na viongozi wasio watumishi wa umma. “Rais Samia atatumia fursa ya mkutano na wazee hao kulihutubia Taifa,” ni mkutano mwafaka, unaorejesha matumaini na kuendelea kuponya pale ambapo Watanzania waliumia” Amesema Chalamila.