Skip to main content

Posts

Showing posts from October 27, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt Judith Mhina Awaomba Watanzania Kuacha Kuchezea Tunu ya Amani

 Taasisi ya Mwanamke na Nguvu ya kijani TANZANIA imewaasa wanawake na vijana kuwa makini katika kulinda amani huku ikiwataka kuwa mabalozi wa amani ili kusaidia kujenga kizazi chenye utu na heshima katika jamii . Hayo yamebainishwa mapema Oktoba 26 mwaka huu 2025, na Mwenyekiti wa Taasisi ya mwanamke na nguvu ya kijani ambaye pia ni Mwenyekiti wa makampuni ya PMM Group Dkt Judith Mhina Spendi katika kongamano la amani la kitaifa lililoandaliwa na taasisi hiyo lenye lengo la kutoa elimu kwa Watanzania kuhusu amani na umuhimu wake katika jamii. Amesema kuwa Tanzania imejijengea sifa ya kuwa nchi ya amani, utulivu na mshikamano kupitia juhudi mbalimbali zinazoendelea kufanywa na Serikari ikishirikiana na wadau nchini katika kuimarisha hali ya amani. Hata hivyo Dkt Judith Mhina amewataka watanzania kutotamani nafasi zisizozao katika jamii kwani kufanyq hivyo ni mojo ya sababu ya kuchochea uvunjifu wa amani katika jamii ya watanzania hasa katika kuelekea siku ya uchaguzi oktoba 29. Ai...

Rai ya Mwandishi wa riwaya za kigiriki Aristophanes

 Leo katika pita pita zangu nikaamua niwasome waandishi wa kigiriki na nikakutana na Mwandishi mashuhuri  aitwaye *Aristophanes* wa riwaya  🖊️ pendwa mbalimbali .  *Aristophanes*  alizungumzia  *wajibu wa Vyombo vya Habari katika Taifa Lenye Mgawanyiko wa Kiimani na itikafi.*  Katika nukuu yake anasema "Vyombo vya habari vina nafasi muhimu katika kujenga na kudumisha umoja wa kitaifa, hususan katika mazingira ambayo taifa linakabiliwa na mgawanyiko wa kisiasa, kijamii au kiitikadi"  Katika hali kama hiyo, wajibu wa vyombo vya habari  havitakiwi  kuchukua upande mmoja wa mgogoro, bali kuwa daraja linalounganisha pande zinazotofautiana. Vyombo vya habari vinapaswa kutumia nguvu yake ya mawasiliano kuhimiza mazungumzo ya wazi, kuheshimiana na kueleza kwa umma umuhimu wa umoja, mshikamano na amani ya kudumu. Kupitia taarifa sahihi, usawa wa maoni na uwajibikaji katika kuripoti, vyombo vya habari vinaweza kuwa chachu ya maridhiano na maendeleo y...

Kukamilika kwa mradi wa Agri-Connect utabadili Taswira ya miundombinu ya Mbinga

# Ni barabara ya Utili–Mahande itakayofungua fursa za kiuchumi kwa wakulima  #Vikundi kazi vinne vyasajiliwa  Mbinga, Ruvuma Katika juhudi za kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Mbinga, Meneja wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani humo, Mhandisi Oscar Musa, amesema mradi wa Agri-Connect unaotekelezwa katika barabara ya Utili–Mahande umefikia hatua muhimu ya ujenzi. Mradi huo wenye urefu wa kilomita 14.4 na thamani ya shilingi bilioni 16.5 ulianza kutekelezwa mwezi Novemba 2024 na unatarajiwa kukamilika Mei 2026, ikiwa ni kipindi cha miezi 18. Kwa sasa, kazi ya kuchonga na kufungua barabara yote imekamilika, huku ujenzi wa madaraja saba ukiendelea sambamba na uwekaji wa tabaka la udongo ambapo kilomita 8 tayari zimekamilika. Mhandisi Musa amesema kwamba mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi kutoka kampuni ya Ovans Construction Ltd iliyoko Mbinga. “Lengo kuu la mradi huu ni kuwahudumia wananchi wa vijiji vya Utili, Mahande na Mbin...

Dkt.Samia Awasili Jijini Mwanza Kufunga Kampeni Kesho

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt.Samia Suluhu Hassan amewasili jijini Mwanza leo Oktoba 27,2025 kwa ajili ya kufunga mikutano  ya kampeni ya chama hicho hapo kesho Oktoba 28,2025 ndani ya jiji la Mwanza. Dkt.Samia amepokewa na Mgombea mwenza wa Urais wa chama hicho Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi,Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Stephen Wasira,Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt.Asha-Rose Migiro pamoja na viongozi  Waandamizi wa chama mkoa wa Mwanza.