Skip to main content

Posts

Showing posts from July 5, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hatua ya Trump kuzima misaada ya USAID itaua watu 14 milioni – Utafiti

 Mataifa 132 Duniani ikiwemo Kenya na Tanzania ambayo yalikuwa yakinufaika moja kwa moja na ufadhili kutoka kwa Shirika la Ustawi wa Kimataifa la Marekani (USAID), ziko hatarini kupoteza jumla ya watu 14 milioni kufikia mwaka 2030 baada ya kufungwa rasmi kwa shirika hilo la kutoa misaada. Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la sayansi la Lancet unaeleza kwa kina jinsi hatua zilizopigwa katika miongo miwili iliyopita kupunguza vifo vya watoto na watu wazima, zitaporomoka. “Makadirio yetu yanaonyesha kuwa, isipokuwa hatua za kupunguza ufadhili zilizotangazwa na kutekelezwa katika nusu ya kwanza ya mwaka 2025 ziondolewe, idadi kubwa ya vifo vinavyoweza kuepukika vinaweza kutokea kufikia mwaka 2030,” walisema watafiti. Tofauti na tafiti za awali ambazo zilijikita tu kwenye athari za moja kwa moja za kiafya, utafiti huu mpya umeangazia pia athari mbadala ambazo pia zinaweza kusababisha vifo na kupoteza njia za kujikimu, na kueleza kuwa pia zinaathiri afya ya watu. Mipango isiyo ya ...

Dkt. Biteko Asema Tanzania ina Usalama wa Chakula, Awapongeza Wakulima

📌 Asema Serikali inatambua Vyama vya Ushirika ni muhimu kuunganisha nguvu za wananchi na kujiendeleza kiuchumi 📌 Mauzo ya nje ya kahawa na tumbaku 2023/2024 yaongezeka hadi Dola za Marekani 19,300,000 📌 Maono ya Rais Samia yaanza kuonekana sekta ya kilimo yachangia GDP asilimia 26 📌 Aziagiza Wizara za Fedha na Kilimo kupata ufumbuzi wa bei za mazao Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewapongeza wakulima nchini kwa jitihada zao za kuzalisha mazao kwa wingi na hivyo  kusaidia nchi kuwa na usalama wa chakula  ikiwa ni pamoja na kuwezesha sekta ya kilimo kuwa na mchango mkubwa katika Pato la Taifa.  Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo Julai 5, 2025 jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano la Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani. “Leo sekta ya kilimo ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi yetu, tunazungumza mchango wa GDP wa asilimia 26, tunazungumza mazao ambayo yanatupa...

Fanyeni Kaguzi Kwenye Maeneo Yaliyohifadhiwa-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Mamlaka za Mikoa na Wilaya kufanya kaguzi za mara kwa mara katika maeneo yaliyohifadhiwa, vyanzo vya maji na mito ili kudhibiti vitendo vya uharibifu wa mazingira. Ametoa agizo hilo leo (Jumamosi Julai 05, 2025) aliposhiriki katika mbio za Great Ruaha Marathon (GRUMA 2025) zilizoanzia na kuishia kwenye eneo la Ibuguziwa, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, mkoani Iringa. “Wekeni utaratibu mzuri wa matumizi ya vyanzo hivyo, tunataka kuona mikondo yote ya maji inayokwenda kulisha mto mkuu, inahifadhiwa ili tupate maji mengi na yaweze kuchangia kwenye shughuli za kimaendeleo, mto Ruaha Mkuu unapeleka maji katika bwawa letu la kuzalisha umeme la Mwalimu Nyerere” Mheshimiwa Majaliwa ameziagiza mamlaka hizo zibainishe vyanzo muhimu vya maji vilivyopo kwenye maeneo yao na kuweka utaratibu maalum na wawazi juu ya namna ya kuhifadhi vyanzo hivyo ili viweze kuzalisha maji ya kutosha. “Mimi ninawasihi wekeni Sheria ndogo zinazodhibiti uharibifu na kutambua ...