Skip to main content

Posts

Showing posts from July 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rushwa na Fitina Chanzo cha Kukatwa Wabunge Majimboni

 Hekaheka za mchujo CCM: Sababu ya wabunge nguli kufyekwa na wajumbe hizi hapa  *Yadaiwa walikuwa bize na wananchi wakasahau 'kuwaona' wajumbe wa kamati za siasa *Wajumbe wengine walia kupunjwa mgao BAADHI ya kamati za siasa za chama cha Mapinduzi CCM za wilaya nchini, zinadaiwa kukiuka taratibu za chama hicho za kuwapata viongozi wa dola kwa madai ya kupokea rushwa, jambo ambalo liliwafanya kuendesha vikao vya mchujo kwa upendeleo mkubwa, chuki na fitna. Uchunguzi ambao umefanywa katika baadhi ya mikoa nchini, umebaini kuwa baadhi ya viongozi wa kamati hizo hasa wenyeviti na makatibu walinunuliwa kabla ya kuanza kwa vikao hivyo vya mapendekezo kwa wagombea ubunge na udiwani. Imeelezwa kuwa chanzo cha viongozi hao kununuliwa na baadhi ya wana CCM, waliokuwa tayari wamejipanga kuchukua fomu ni kutokana na baadhi ya wabunge kushindwa kuwajali binafsi badala yake walitumia muda mwingi kwa shughuli za maendeleo pamoja na kuwalinda wajumbe katika maeneo hayo. Imeelezwa kuwa kutok...

Majaliwa Amwakilisha Rais Dkt. Samia Ibada ya Kuwekwa Wakfu Askofu Mteule Dkt. Daniel Mono

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo Julai 13, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kumweka wakfu na kumuingiza kazini Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mwanga. Ibada hiyo imefanyika katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Rais Museveni Aagiza Kufukuzwa Kazi wafanyakazi 152 wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe

Rais wa Uganda Jenerali Mstaafu Yoweri Kaguta Museveni ameagiza Mamlaka ya usafiri wa anga nchini humo(UCAA)kuwafukuza kazi mara moja wafanyakazi 152 walioajiriwa na Mamlaka hiyo bila kuwa na sifa stahiki. Kwa mujibu wa Rais Museveni, wafanyakazi wanaotakiwa kufukuzwa walipata ajira kupitia Rushwa na hivyo kuchangia kuwepo kwa huduma duni katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Entebbe.  "Nimepokea Taarifa kuhusu Kushamiri kwa Rushwa katika Mamlaka ya UCAA ikiwemo Utoaji wa ajira kwa watu wasio na sifa na Matokeo yake kusababisha matatizo ambayo hayapaswi kuachwa kuendelea , Miongoni mwa matukio ya aibu na Fedheha ni kukwama kwa Mama Maria Nyerere katika lifti ya Uwanja wa Ndege wa Entebbe kwa muda wa dakika nne,Uchunguzi umefanyika na kubaini wafanyakazi 152 hawana sifa ambapo Naamuru wote wafukuzwe pamoja na wale wote waliowaajiri na nahitaji hilo litekelezwe kwa haraka sana"Rais Museveni alieleza katika Barua yake kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi wa Uganda Jenerali Edward K...

Sichezi mtakiona, Ruto aonya upinzani akisitiza amri ya waporaji kupigwa risasi

Huku mashirika mbalimbali ya kimataifa, ikiwemo Umoja wa Mataifa na makundi ya kutetea haki za binadamu, yakishutumu polisi Nchini Kenya kwa kutumia nguvu kupita kiasi katika maandamano ya hivi karibuni dhidi ya serikali, Rais William Ruto  Jumamosi alisisitiza msimamo wake wa kuamuru watu kupigwa risasi mguuni. Rais Ruto ameahidi kulinda maisha na mali za Wakenya kwa nguvu zote huku akilaumu upinzani kwa kuchochea vijana kuzua vurugu. Akizungumza katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet,Rais Ruto alisema atachukua hatua kali dhidi ya wahalifu wanaolenga mali za watu, ikiwa ni pamoja na wizi na uporaji. Aidha, alitaka viongozi wa kidini na wanasiasa wasitafsiri hatua kali dhidi ya waandaji wa  ghasia katika maandamano ambayo yamesababisha vifo kadhaa na uharibifu mkubwa wa mali, kama mateso ya kisiasa. “Nimevumilia kwa muda mrefu sana, sasa imetosha. Wale mnaochochea vijana kuingia kwenye ghasia mtawajibika, msije mkasema ni mateso ya kisiasa,” alisema Rais Ruto wakati wa hafla ya kup...

Jenerali Mstaafu Waitara: Changamkieni Fursa za Uwekezaji - Hifadhi za Kusini.

Na: Happiness Sam – Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini TANAPA - Jenerali mstaafu George Waitara amewahamasisha wawekezaji kuwekeza katika mazao ya utalii pamoja na malazi hususani katika Hifadhi za Kusini zilizojaliwa kuwa na hazina lukuki ya wanyamapori ili kuvutia watalii wengi kwa lengo la kuliongezea Taifa mapato. Hayo aliyasema leo Julai 12, 2025, alipotembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Jenerali Waitara alisema, “Ukanda wa Kusini una hazina kubwa ya vivutio vya kipekee ambavyo vinaweza kuwa kichocheo kikubwa cha uchumi na utalii endapo vitawekewa nguvu ya uwekezaji na kutangazwa kikamilifu, ni muda muafaka sasa kwa sekta binafsi kushirikiana na Serikali kupitia TANAPA katika kuibua na kuendeleza maeneo hayo, ili kupanua wigo wa kitalii na kuongeza pato la Taifa kupitia sekta hiyo”. “Kama ilivyozoeleka wawekezaji wengi wa sekta ya utalii wamewekeza sana upande wa K...