Skip to main content

Posts

Showing posts from February 24, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mtambi Awataka Wananchi Kutatua Changamoto Kwa Amani

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi akiambatana na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara ametembelea eneo lenye mgogoro wa ardhi katika mpaka wa Kata ya Mwema na Regicheri, Wilaya ya Tarime na kuwataka wananchi kujifunza kutatua changamoto zao kwa amani.  “Sio kila changamoto inahitaji utatuzi wa kutumia nguvu na mapanga, changamoto nyingine zinazungumzika kwa amani na utulivu na inapatikana suluhu ya kudumu” amesema Mhe. Mtambi na kuongeza kuwa “hapa hamna mshindi wala bingwa katika mgogoro huu”.   Mhe. Mtambi amewataka wananchi kuhakikisha kuwa mgogoro huu unatatuliwa kwa amani na utulivu na kuwahakikishia wakiendelea na mgogoro huo atatoa kipande kinachogombewa kwa uongozi wa JKT ili wenye mashamba katika eneo hilo wafanye kazi chini ya uongozi wa kijeshi.  Mhe. Mtambi amemwagiza Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Mara kutambua mpaka wa Kata hizo na kuuangalia mpaka wa Inglam uliowekwa na Serikali ya Wakoloni sambamba na utambuzi wa wamiliki halali wa...

Nawapenda Wananchi Wa Bumbuli,Lushoto Mjini,Mkomazi na Korogwe Mjini -Rais Samia

 Imekuwa Jumatatu nzuri ya kazi na wananchi Bumbuli, Lushoto Mjini, Mkomazi na kisha Korogwe Mjini, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yangu ya kikazi katika Mkoa wa Tanga.  Mbali na kuupa Mkoa wa Tanga Shilingi Trilioni 3.1 kwa miradi ya maendeleo katika kipindi cha miaka minne ambayo sasa tunaona matokeo yake kwenye maisha ya wananchi, tumeanza ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji Mkomazi, moja ya miradi muhimu kwa watu wa Mkoa wa Tanga hasa kwenye kilimo.  Katika Wilaya ya  Korogwe pekee, mradi huu utanufaishi zaidi ya wananchi 20,000, na kuwapa nafasi ya kukua zaidi katika kilimo cha mazao ya chakula na biashara.

Waziri Mkuu Atoa Pole Kwa Waziri Mchengerwa

  Waziri Mkuu Kaassim Majaliwa akimpa pole Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa aliyefiwa na Baba yake yake mzazi, Omari Rashid Mchengerwa, nyumbani kwa Waziri huyo Masaki jijini Dar es salaam February 24, 2025. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na waombolezaji alipokwenda nyumbani kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mohammed Mchengerwa, Masaki jijini Dar es salaam kutoa pole ya kifo cha Baba mzazi wa Waziri huyo, marehemu Rashid Mchengerwa, February 24, 2025.  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Omari Rashid Mchengerwa, Baba mzazi wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mohammed Mchengerwa, nyumbani kwa Waziri huyo Masaki jijini Dar es salaam, Februari 24,2025. 

Waziri Kikwete Azindua Miradi Yenye Thamani Ya Shilingi Bil.1.6 Wilayani Songwe

*Wananchi wamshukuru Rais Samia kwa kutenga fedha za miradi  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi , Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amezindua miradi ya Elimu, Umeme na barabara yenye thamani ya shilingi bilioni 1.6 katika Halmashauri ya wilaya ya Songwe mkoani Songwe  Akiongea wakati wa uzinduzi wa Miradi hiyo  leo tarehe 24 Februari 2025, amesema Mradi wa Ujenzi wa shule ya Maweni B ambao umegharimu shilingi milioni 583 utasaidia kuondoa adha  ya kutembea umbali mrefu kwenda shule kwa  watoto wa Mkwajuni, kupunguza msongamano darasani pamoja na utoro wa rejareja. Mhe.Kikwete amezindua  pia madarasa Sita yatakayotumika kwa kidato cha Tano na Sita katika shule ya sekondari Kanga. Mradi huo  wenye thamani ya shilingi milioni 150 utawezesha pia vijana kuishi bweni na  kuboresha mazingira ya malazi na Ujifunzaji kwa wanafunzi. Amezindua ujenzi wa barabara za Mkwajuni mjini kwa Kiwango cha lami wenye thamani ya shilingi mili...

Mahusiano ya Kidiplomasia Yametunufaisha-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema jitihada za kujenga mahusiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi washirika zinazofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan zimekuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania. "Tangu aingie madarakani  Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amekuwa kinara katika kujenga mahusiano na nchi mbalimbali jambo ambalo limeleta heshima kubwa na manufaa kwa nchi yetu hususan kwa kufungua fursa za kibiashara na uwekezaji kutoka  nchi washirika". Ameyasema hayo leo (Jumatatu Februari 24, 2025) alipokutana na ujumbe wa wabunge wa bunge la Ulaya  (EU) kutoka Kamati ya Ushirikiano na Maendeleo  kwenye Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam. Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amebainisha kuwa Umoja wa Ulaya umeendelea kuwa mdau mkubwa wa Tanzania katika kukuza biashara na uwekezaji kupitia nchi washirika. "Tanzania inathamini ushirikiano wa kiuchumi na kidemokrasia uliopo kati ya Tanzania na nchi za Umoja wa Ulaya." Amesema biash...

Rais Samia Aagiza Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji Mkomazi Ukamilike Kwa Wakati

Na NIRC ;Tanga. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameeleza kuridhishwa kwake na maendeleo ya mradi wa Umwagiliaji Mkomazi unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) mkoani Tanga. Akizungumza wakati wa uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa Bwawa la Umwagiliaji Mkomazi, Dk. Samia amesema kuwa mradi huo uliozungumzwa kwa miaka mingi bila ya kufanyiwa  kazi, lakini sasa serikali imeamua kuujenga na kueleza kuridhishwa na hatua ya ujenzi wa mradi.  “Ni matarajio yangu kuwa itakapokamilika miradi hiyo kero ya maji itakuwa ni historia huku Lushoto, bwawa hili likikamilika litakuwa na uwezo wa kuingiza maji zaidi ya lita bilioni 70 kwa ajili ya kilimo,”alisema. Amesema lengo la ujenzi wa bwawa hilo ni kutumika katika shughuli za kilimo na mambo mengine lakini kubwa ni uzalishaji wa mazao ya kilimo. Rais Samia amesisitiza kuwa Tanzania sasa inajitegemea kwa mazao ya chakula kwa asilimia 128 huku Nchi zinazoizunguka Zikiwa hazijitoshelezi kwa chakula na hivyo kutoa fursa ya Soko la...