Na. Beatus Maganja Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Nchini - TAWA Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis Semfuko amewahimiza watanzania kuchangamkia fursa za ufugaji wa wanyamapori zinazopatikana katika Taasisi ya TAWA. Ameyasema hayo Julai 13, 2024 alipotembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii Katika Maonesho ya 48 ya biashara ya Kimataifa ambayo kwa Mwaka 2024 leo yamefikia tamati. "Sehemu kama Afrika ya Kusini ufugaji wa wanyamapori ni mkubwa sana, kwahiyo mimi natoa rai kwa wananchi hasa watanzania kuingia katika biashara hiyo ya ufugaji wa wanyamapori" amesema. Aidha Meja Jenarali (Mstaafu) Semfuko amesema ili watanzania waweze kupata kitoweo cha nyamapori kwa urahisi wanapaswa kuingia katika biashara ya ufugaji wa wanyamapori na kwakufanya hivyo wataziwezesha bucha za wanyamapori kufanya kazi vizuri. Sambamba na hilo, Semfuko amesema TAWA ina mipango mingi ya kuhakikisha inapata wawekezaji wakubwa na wadogo ili wawekeze katika maeneo ...
Marato tv - Sauti ya Jamii