Na Mashaka Mhando, TANGA UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Tanga Mjini umepata ugeni mzito kutoka ngazi ya Taifa, katika ziara iliyolenga kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan uwezeshaji wa wanawake kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Serikali. Ziara hiyo iliyofanyika jana, Agosti 5, 2026, iliongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT Taifa ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga, Mhe. Husna Sekiboko. Lengo kuu la ufuatiliaji huo ilikuwa ni kujionea kwa vitendo namna mabilioni ya fedha yanayotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, yanavyoendelea kuboresha maisha ya wananchi, hasa wanawake na makundi maalum. Ukaguzi wa Miradi ya asilimia 10 Akiwa wilayani humo, msafara wa Mhe. Sekiboko ulianza kwa kutembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Nyumba ya Mtumishi wa UWT lililopo Mtaa wa Amboni Kihongwe, katika Kata ya Mzizima. Baada ya hapo, viongozi hao walifanya ziara ...