Skip to main content

Posts

Showing posts from March 14, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mbunge Ghati Chomete Aendelea Kushiriki Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Ghati Zephania Chomete ameendelea kushiriki katika shughuli za **Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo**, ambayo tarehe 14 Machi ilifanya ziara ya kikazi katika Kituo cha Uhakiki cha Misugusugu kilichopo Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani. Ziara hiyo ya Kamati iliongozwa na Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Deodatus Philip Mwanyika, ikiwa na lengo la kukagua mradi wa Wakala wa Vipimo (WMA) pamoja na kujionea utekelezaji wa majukumu ya wakala huo katika kuhakikisha usahihi wa vipimo vinavyotumika nchini. Katika ziara hiyo, Kamati ilikagua mitambo mbalimbali inayotumika katika uhakiki wa vipimo, ikiwemo mitambo ya uhakiki wa mita za umeme, mita za maji pamoja na mifumo ya uhakiki wa matenki ya kupimia mafuta. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa vipimo vinavyotumika katika shughuli za kiuchumi vinakuwa sahihi ili kulinda haki za watumiaji na wafanyabiashara. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Deodatus Phil...

Waziri Mkuu Asisitiza Amani, Maadili na Ushirikiano na Taasisi za Dini

_Asema Taasisi Za Dinidini nguzo ya maadili na amani nchini_ _Aonya migogoro ya ardhi inaweza kuvuruga mshikamano wa Taifa_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini nchini katika kulinda amani, kuimarisha maadili na kuchochea maendeleo ya Taifa. Dkt. Mwigulu amesema hayo leo Jumapili (Machi 15, 2026) wakati akitoa salamu katika Ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Mpanda Mjini, Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, iliyoongozwa na Askofu Imani Ahobokile Chibona. Amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za dini katika kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu, upendo, haki na uwajibikaji. “Nimekuja pia na salamu za upendo kutoka kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kudumisha amani, maadili mema na mshikamano wa kitaifa,” amesema. Waziri Mkuu amesema taasisi za dini zim...

Bunge Lakoshwa TRC Kuwa Taasisi ya Kwanza Kwa Nchi za Afrika Kuunda Vichwa Vya Treni za MGR Yenyewe

  Kamati ya Bunge ya  Kudumu ya Miundombinu, imelitolea wito Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuendelea kuwajengea uwezo vijana wa Kitanzania wanaounda na kukarabati vichwa vya treni za MGR, kwa kuwapa mafunzo thabiti ndani na nje ya nchi ili kuongeza maarifa, stadi na ubunifu katika utendaji wao kazi hiyo  . Wito huo umetolewa Machi 14, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya  Kudumu ya Miundombinu Mhe. Selemani Kakoso,  wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenga kukagua mradi wa uundaji wa vichwa vya treni za MGR, unaoendelea katika karakana ya Pugu, Jijini Dar es Salaam.  Mheshimiwa Kakoso kwa niaba ya kamati hiyo, ameitaka TRC kuhakikisha  inawapa fursa na kuwapeleka vijana hao wenye ujuzi nje ya nchi kujifunza  na kuchota utalaamu zaidi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao, aidha alitoa rai kwa TRC  kuwapa k kipaumbele katika suala la ajira  ili waendelee kulitumikia shirika na nchi kwa uaminifu. Aidha Mhe. Kakoso, alisema kamati ...

Bunge Lakoshwa TRC Kuwa Taasisi ya Kwanza Afrika Kuunda Vichwa vya SGR Yenyewe

  Kamati ya Bunge ya  Kudumu ya Miundombinu, imelitolea wito Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuendelea kuwajengea uwezo vijana wa Kitanzania wanaounda na kukarabati vichwa vya treni za MGR, kwa kuwapa mafunzo thabiti ndani na nje ya nchi ili kuongeza maarifa, stadi na ubunifu katika utendaji wao kazi hiyo  . Wito huo umetolewa Machi 14, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya  Kudumu ya Miundombinu Mhe. Selemani Kakoso,  wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenga kukagua mradi wa uundaji wa vichwa vya treni za MGR, unaoendelea katika karakana ya Pugu, Jijini Dar es Salaam.  Mheshimiwa Kakoso kwa niaba ya kamati hiyo, ameitaka TRC kuhakikisha  inawapa fursa na kuwapeleka vijana hao wenye ujuzi nje ya nchi kujifunza  na kuchota utalaamu zaidi ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao, aidha alitoa rai kwa TRC  kuwapa k kipaumbele katika suala la ajira  ili waendelee kulitumikia shirika na nchi kwa uaminifu. Aidha Mhe. Kakoso, alisema kamati ...