Skip to main content

Posts

Showing posts from September 14, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Awapa Kazi Viongozi wa Mkoa wa Kagera

 Na Angela Sebastian; Biharamulo  Kuongozi wa mbio za mwenge Kitaifa Ismail Ali Ussi amewataka mkuu wa mkoa wa Kagera,wakuu wa Wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri zote na Manispaa ya Bukoba kuwahamasisha wananchi kutumia Nishati safi ili kuepukana na athari za kiafya zitokanazo na nishati chafu. Ametoa ushauri huo akiwa Wilayani Biharamulo ambapo amesema viongozi hao wanakumbuka kwamba Rais Dk Samia Suluhu Hassan amekuja na kampeni ambayo ina lengo la kuwasaidia wananchi wa Tanzania ikiwemo Biharamulo ambapo inaenda kuwajali na kuwagusa wananchi moja kwa moja kwa kuweka Afya zao kuwa imara. "Dk.Samia amekuja na utaratibu wa uhamasishaji wa matumizi ya gesi na Nishati safi mbadala katika maeneo mbalimbali ndani ya Taifa hili ,ndiyo maana yapo maelezo yaliyotolewa kwa wakuu wa mikoa,Wilaya na wakurugenzi kuwataka wahamasishe kampeni hiyo katika maeneo ambayo yana mkusanyiko wa kuanzia watu 100 na kuendelea ikiwa ni ya binafsi au Serikali kuhakikisha wanatumia gesi ambapo shu...

Ndege ya Rais Kenya, Harambee One, Kustaafishwa Baada ya Miaka 30

Nairobi, Kenya   Serikali ya Kenya imetangaza kuwa ndege ya rais, maarufu kama Harambee One, itastaafishwa rasmi baada ya kutumika kwa zaidi ya miongo mitatu.  Habari zinabainisha kwamba ndege hiyo aina ya Fokker-70 hivi sasa iko kwenye safari yake ya mwisho ya matengenezo makubwa nchini Uholanzi. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Harambee One imekumbwa na changamoto nyingi za kiufundi kwa miaka ya karibuni, ikiwa ni pamoja na matatizo ya mfumo wa majimaji (hydraulic system), milango kushindwa kufunguka ipasavyo, pamoja na gharama kubwa za matengenezo.  Aidha, upatikanaji wa vipuri vya ndege hiyo umekuwa mgumu kutokana na umri wake, jambo lililochangia uamuzi wa serikali kuiondoa kwenye huduma. Waziri wa Ulinzi Bi.Soipan Tuya amenukuliwa akisema "Harambee One imelitumikia taifa kwa heshima na uaminifu kwa zaidi ya miaka 30. Lakini sasa tumefikia wakati ambapo gharama za kuiendesha zimekuwa kubwa kuliko thamani yake.Sheria inaturuhusu kubadilisha ndege ya Rais kila baada ya...

Riek Machar Ashtakiwa kwa Uhaini Sudan Kusini

Juba, Sudan Kusini  Hali ya kisiasa nchini Sudan Kusini imeingia katika mtafaruku mpya baada ya serikali kutangaza rasmi mashtaka ya uhaini dhidi ya Makamu wa Kwanza wa Rais aliyesimamishwa, Riek Machar Teny. Mashtaka hayo mazito yanajumuisha uhaini, mauaji, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita, kutokana na mashambulizi ya Machi mwaka huu katika mji wa Nasir, Jimbo la Upper Nile na kusababisha vifo vya said ya wanajeshi Mia mbili. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mwendesha Mashtaka Mkuu, mashambulizi hayo yalitekelezwa na wanamgambo wa White Army ambapo watu kadhaa waliuawa na mamia kujeruhiwa.  Serikali ya Rais Salva Kiir Mayadit inadai kuwa mashambulizi hayo yalikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Machar, ambaye kwa muda mrefu ameonekana kama kiongozi wa kisiasa mwenye ushawishi mkubwa miongoni mwa wapiganaji hao. “Ushahidi wetu unaonyesha wazi kwamba Dkt. Machar alihusika katika kuratibu na kusapoti mashambulizi hayo. Serikali haiwezi kukaa kimya mbele ya vitendo...

Ccm Inawagombea Bora na lmara-Majaliwa

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinawagombea bora na imara wenye uwezo wa kuendelea kuleta maendeleo nchini. Amesema kuwa safu hiyo inaongozwa na mgombea wa Urais wa CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye katika kipindi chake kinachoishia amefanya mambo mengi na makubwa ambayo yamewanufaisha na kugusa maisha ya kila siku ya watanzania. Amesema hayo leo Jumapili (Septemba 14, 2025) wakati wa Uzinduzi wa Kampeni za ubunge wa jimbo la Lindi Mjini zilizofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mnazi Mmoja mkoani Lindi. “Rais Dkt. Samia amefanya kazi kubwa nchini ikiwemo katika mkoa wetu wa Lindi, hatuwezi pata mafanikio kama hatuwezi kuwa na muendelezo wa uongozi, Rais huyu ameleta fedha za miradi, upo umuhimu wa kumuongezea muda ili yale aliyoyaanza ayaendeleze, tunamuachaje Rais Dkt. Samia? kwanini tumuache?” alihoji Mheshimiwa Majaliwa Ameongeza kuwa watanzania hawana sababu ya kuwa na mashaka na R...

Dkt Nchimbi Awashukuru Wana Kilimanjaro Akihitimisha Kampeni Zake Mkoani Humo

MGOMBEA Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John  Nchimbi, amepokewa kwa shangwe na Wananchi Kata ya Ndungu, Jimbo la Same Mashariki,alipowasili katika uwanja wa kata hiyo  kwenye mkutano wake wa mwisho wa kampeni Mkoani Kilimanjaro leo Jumapili Septemba 14,2025. Dkt.Nchimbi aliwanadi Wagombea Ubunge wa Mkoa huo akiwemo Mgombea Ubunge wa Jimbo la Same Mashariki,Ndugu Anne Kilango Malecella pamoja na Madiwani. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri Mkuu na Makamu Wa Rais mstaafu Mzee John Samuel Malecela ambaye ni mume wa Mama Anne Kilango.

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Yahimiza Uhifadhi wa Mto Mara

📍 *Butiama, Mara.* Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC)  imehimiza kuhusu uhifadhi wa mto Mara ili Kuuwezesha kudumu na kuwa endelevu  Hayo yamejiri wakati wataalamu wa Tume wakiendelea kutoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mara, katika Maadhimisho ya Siku ya Mto Mara (Mara Day), yanayofanyika kuanzia Septemba 12 hadi 15 mwaka huu kwenye Viwanja vya Mwenge, Wilaya ya Butiama, Mkoa wa Mara. Katika maadhimisho hayo, Tume pia inatoa elimu kwa wananchi kuhusu Sheria ya Taifa ya Umwagiliaji, ada ya huduma za umwagiliaji na teknolojia za kisasa za umwagiliaji, sambamba na kusisitiza umuhimu wa utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji. Mto Mara ni kiunganishi kinachosaidia ustawi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini Tanzania na Maasai Mara nchini Kenya, ambapo kila mwaka mamilioni ya wanyama wahamao hupita katika eneo hilo, ikiwa ni urithi wa dunia unaotegemea uhai wa bonde hilo. Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Mara, Mhandisi Adelialidy Mwesiga, amesema miongoni mwa jitihada zinazot...