Skip to main content

Posts

Showing posts from March 13, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Watumishi Wlwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Watakiwa Kuendelea Kuzingatia Maadili ya Utumishi wa Umma

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari amewataka Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma ili waweze kutoa huduma bora kwa Wananchi.  Mwanasheria Mkuu wa Serikali amezungumza hayo wakati  akifungua Mafunzo elekezi kwa Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yaliyofanyika tarehe 13 Machi, 2025 Jijini Dodoma. Akizungumza wakati akifungua Mafunzo hayo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewakumbusha Watumishi umuhimu wa utoaji wa huduma za ushauri wa kisheria, ushughulikiaji wa malalamiko ya wananchi kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali ambayo imetolewa wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.  *“Tunatakiwa kuendelea kuzingatia Sheria na Kanuni tulizojiwekea ili tuweze kutoa huduma bora na stahiki kwa wananchi.”* Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Aidha, Mhe. Johari amewahimiza Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kusoma Mpango Kazi w...

Waziri Mkuu Akiwaaga Viongozi wa Mkoa Tabora

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Machi 14, 2025 akiagana na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) baada ya kumaliza ziara ya siku mbili katika mkoa wa Tabora kwenye wilaya za Nzega na Igunga.

Tanzania yang’ara Katika Utekelezaji Wa Shughuli za Uwazi na Uwajibikaji Katika Sekta ya Madini

  📍Arusha. SERIKALI imesema itaendelea kuweka wazi taarifa za uwekezaji na mapato yanayopatikana katika sekta ya Madini, Mafuta na Gesi Asilia nchini kama Sheria inavyotaka na kwa kuzingatia vigezo vya Uwazi na Uwajibikaji vinavyosimamiwa na  Asasi ya Kimataifa ya EITI.  Hayo yameelezwa leo Machi 13, 2025 na Mhe. Innocent Bashungwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wakati akifungua akifungua mkutano wa 62 wa bodi ya Kimataifa ya Uwazi na Uwajibikaji (EITI), ulioanza jana jijini Arusha. Waziri Bashungwa amesema wananchi wanapaswa kufuatilia na kujua mambo yanayoendelea katika sekta ya Madini, Mafuta na Gesi Asilia, Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa mapato hayo yanawekwa wazi kwa lengo la kuimarisha  uaminifu kwa wananchi. Aidha, Waziri Bashungwa amesema "Kwa kuzingatia Tanzania ni mwanachama wa bodi ya EITI inayosimamia Uwazi na Uwajibikaji, Mwaka 2015 Serikali ilitunga Sheria ya kusimamia Uwazi na Uwajibikaji  katika rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia, ...

Almasi, dhahabu yaipaisha Shinyanga

  🟠*Yafikia 82% ya lengo ukusanyaji maduhuli* ·  *Fursa bado zipo njooni - Mapunda*  *Shinyanga* MAKUSANYO  ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Shinyanga  yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha  ulioanza Julai 2024/ 2025 ni Shilingi Bilioni 21.5  Mkoa wa Shinyanga ulipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 26.2 ambapo mpaka mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu  umefanikiwa kukusanya kiasi hicho cha fedha ambacho ni sawa na asilimia 123 katika kipindi cha miezi nane na asilimia 82 ya lengo la mwaka. Akizungumza katika mahojiano maalum, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Shinyanga, Mjiolojia Daniel Mapunda amesema fedha hizo zimekusanywa kutokana na  jitihada mbalimbali walizofanya katika usimamizi wa sekta.  “Mwenendo ni mzuri, hadi kufikia mwisho wa mwaka wa fedha tuna imani tutafikia lengo,” amesema Mapunda. Aidha, Mapunda ametoa wito kwa wawekezaji kote nchini kuchangamkia fursa za uwekezaji...