Naibu Waziri wa Madini Mhe. Dkt. Steven Kiruswa ametatua mgogoro wa wachimbaji wadogo wa Madini ya Ruby Wilaya ya Longido Mkoani Arusha uliodumu zaidi ya miaka mitano kati ya Kampuni ya Paradiso Mineral (T) Limited na Mzee Malulu Ole Moringo kwa Kampuni hiyo kukubali kumlipa fidia Mzee Malulu Ole Moringo ya jumla ya shillingi milioni miamoja na hamsini ili kupisha shughuli za uchimbaji madini. Makubaliano hayo yameafikiwa leo Desemba 6, 2025 wakati Mhe. Dkt. Kiruswa alipofanya ziara ya kutatua mgogoro huo katika Kata ya Mundarara Wilaya ya Longido Mkoani Arusha. Mhe. Dkt. Kiruswa ameielekeza kampuni ya Paradiso kutekeleza makubaliano walioafikiana na Mzee Malulu Ole Moringo ya kulipa fidia hiyo kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza wanatakiwa kulipa milioni 100 ifikapo Januari 30, 2025 na milioni 50 ifikapo Machi 30, 2025. Aidha, Dkt. Kiruswa amesisitiza makubaliano hayo kutekelezwa kwa wakati na endapo kampuni ya Paradiso itakiuka makubaliano hayo Serikali itachukua hatua za kis...
Marato tv - Sauti ya Jamii