Skip to main content

Posts

Showing posts from June 8, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

ZUNGU ASISITIZA KASI YA UJENZI WA SHULE YA MFANO YA CRDB UPANGA

 Mbunge wa Jimbo la Ilala na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu, amemtaka mkandarasi anayejenga Shule ya Sekondari ya Mfano ya CRDB iliyopo Kata ya Upanga Mashariki jijini Dar es Salaam kuongeza kasi ya ujenzi ili mradi huo ukamilike kwa wakati na kuanza kutumika Januari 2027. Mhe. Zungu ametoa maelekezo hayo Juni 7, 2026 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo akiwa ameambatana na TullyEsther Mwambapa. Akizungumza katika ukaguzi huo, Mhe. Zungu ameipongeza CRDB Bank chini ya uongozi wa Abdulmajid Nsekela kwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha sekta ya elimu nchini. Amesema mradi huo wenye thamani ya takribani shilingi bilioni tano ni uwekezaji muhimu utakaosaidia kuongeza upatikanaji wa elimu bora kwa wanafunzi wa Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi. Kabla ya ukaguzi huo, Mhe. Zungu alishiriki mkutano wa kikanuni wa maendeleo wa wananchi wa Kata ya Upanga...

CCM IMEAGIZA KERO YA MAJI IMALIZWE HARAKA WILAYANI SAME

*Asisitiza Tsh Trilioni 1.2 zimewekezwa Kilimanjaro, sasa ni zamu ya mfumo wa Usambazaji.* MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Baraa, Stephen Wasira, ameiagiza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Same (SAUWASA) kuhakikisha inatatua kwa haraka changamoto ya upatikanaji maji inayowakabili wananchi wa mji wa Same. Wasira alitoa agizo hilo leo Juni 8, 2026 alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM wa Shina Namba 9, Tawi la Same, Kata ya Same, wilayani Same mkoani Kilimanjaro. Akijibu malalamiko ya wananchi kuhusu ukosefu wa maji, alisema haikubaliki kwa wakazi wa Same kuendelea kukosa huduma hiyo muhimu wakati maji yanapatikana kwa wingi kupitia miradi iliyotekelezwa na serikali. “Ninaiagiza SAUWASA kuhakikisha wananchi wa Same wanapata maji. Haiwezekani watu wa Same waendelee kuyasikia au kuyaona maji bila kuyapata kwa matumizi yao ya kila siku, mfumo wa usambazaji uharakishwe ili wananchi wanufaike na huduma hiyo muhimu,” alisema Wasira. Alibainisha kuwa, serika...

AHMED ALLY WA SIMBA ATOA MAAGIZO HAYA HUKO MKOANI KAGERA

 Na Angela Sebastian ;Muleba ‎MSEMAJI wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amemtaka mwaandaaji wa Mashindano ya Mwijage Cup ambayo yanahusisha timu 20 za ndondo kutoka katika Tarafa ya Kamachumu Wilayani Muleba mkoani Kagera, kuyafanya kwa malengo ya muda mrefu na yawe yenye kuibua vipaji kuliko kusubiri muda wa kuomba kura au jambo fulani linalohusu maslahi binafsi. Ally ametoa rai hiyo jana wakati akizindua mashindano hayo katika uwanja wa mpira wa polisi Kamachumu ulioko katika kata ya Kamachumu ambayo yanalenga kuwasaidia vijana kujengewa uwezo wa kucheza mpira wenye viwango vya kimataifa,kuinua vipaji na kutengeneza vipaji vipya kwenye mpira wa miguu kutoka ngazi za chini watakaokwenda kucheza kwenye timu kubwa hapo baadaye. "Mwanzilishi na mdhamini wa mashindano haya (Paul Mwijage) jamii mnapaswa kumuunga mkono ili aendeelee kuwafanyia mema wana michezo hasa wakazi wa Tarafa Kamachumu kwani malengo yake ni kuwaunganisha nyinyi hususani vijana kupitia michezo hivyo yawe endelevu...

ZUNGU:AITAKA NHC KUJENGA NYUMBA ZA BEI NAFUU ILALA

Mbunge wa Jimbo la Ilala na Spika wa Bunge, Mussa Zungu, ameibeba ajenda ya makazi na ustawi wa wananchi kwa kuitaka NHC kujenga nyumba za gharama nafuu zitakazowawezesha wananchi wa kipato cha chini na cha kati kupata makazi bora bila kubanwa na gharama kubwa za upangaji. Akizungumza katika mkutano wa wananchi wa Mitaa ya Kibasila na Kitonga, Kata ya Upanga Mashariki, Zungu alisema maendeleo ya miji yanapaswa kwenda sambamba na kulinda maslahi ya wananchi, akisisitiza kuwa uwekezaji wa makazi usiwe chanzo cha kuwaondoa au kuwaumiza wananchi waliotegemea nyumba hizo kwa miaka mingi. "Tunataka maendeleo yanayowajali wananchi. Nyumba za gharama nafuu zinawezekana na zina hadhi. NHC inapaswa kujenga nyumba zitakazowapa wananchi fursa ya kuishi kwa heshima na usalama," amesema Zungu. Katika mkutano huo, wananchi waliwasilisha kero mbalimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu ya maji, ukosefu wa vivuko salama vya waenda kwa miguu katika maeneo ya shule pamoja na changamoto zinazowak...

SAMIA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Juni 8, 2026 ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimewakutanisha mawaziri wa Serikali kwa ajili ya kujadili na kufanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya taifa, uchumi na ustawi wa wananchi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika kuendelea kuimarisha huduma na maendeleo nchini.

TAKUKURU YAFICHUA MRADI WA SHULE ULIOKWAMA KWA SABABU YA NeST

     NA MASHAKA MHANDO, Tanga TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga, imefichua kukwama kwa miaka miwili kwa mradi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Sekondari Chongoleani Jijini Tanga. Mradi huo wa thamani ya Sh. 93,816,506, ulishindwa kuanza utekelezaji tangu fedha zilipotolewa Machi 4, 2024 kutokana na kasoro kubwa za kiutawala na mfumo wa manunuzi wa halmashauri ya Jiji la Tanga. Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhani Ndwata, aliwaambia waandishi wa Habari ofisini kwake Leo Juni 8 2026 wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa robo ya kwanza ya mwaka (Januari–Machi, 2026), ambapo alisema uingiliaji kati wa taasisi hiyo umeokoa hasara ya jumla ya Sh. 116,216,506 katika sekta ya elimu.  Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa, makadirio ya bei ya vifaa vya ujenzi wa madarasa hayo mawili yalikuwa chini ya bei halisi ya soko, hali iliyosababisha mfumo wa manunuzi wa kielektroniki wa Serikali (*NeST*) kukataa zabuni zote na kukwamisha maendeleo...

lTAKUKURU YAFICHUA MRADI WA SHULE ULIOKWAMA KWA SABABU YA NeST

    NA MASHAKA MHANDO, Tanga TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga, imefichua kukwama kwa miaka miwili kwa mradi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Sekondari Chongoleani Jijini Tanga. Mradi huo wa thamani ya Sh. 93,816,506, ulishindwa kuanza utekelezaji tangu fedha zilipotolewa Machi 4, 2024 kutokana na kasoro kubwa za kiutawala na mfumo wa manunuzi wa halmashauri ya Jiji la Tanga. Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhani Ndwata, aliwaambia waandishi wa Habari ofisini kwake Leo Juni 8 2026 wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa robo ya kwanza ya mwaka (Januari–Machi, 2026), ambapo alisema uingiliaji kati wa taasisi hiyo umeokoa hasara ya jumla ya Sh. 116,216,506 katika sekta ya elimu.  Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa, makadirio ya bei ya vifaa vya ujenzi wa madarasa hayo mawili yalikuwa chini ya bei halisi ya soko, hali iliyosababisha mfumo wa manunuzi wa kielektroniki wa Serikali (*NeST*) kukataa zabuni zote na kukwamisha maendeleo ...

TAKUKURU YAFICHUA MRADI WA SHULE ULIOKWAMA KWASABABU YA NeST

   NA MASHAKA MHANDO, Tanga TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Tanga, imefichua kukwama kwa miaka miwili kwa mradi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Sekondari Chongoleani Jijini Tanga. Mradi huo wa thamani ya Sh. 93,816,506, ulishindwa kuanza utekelezaji tangu fedha zilipotolewa Machi 4, 2024 kutokana na kasoro kubwa za kiutawala na mfumo wa manunuzi wa halmashauri ya Jiji la Tanga. Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga, Ramadhani Ndwata, aliwaambia waandishi wa Habari ofisini kwake Leo Juni 8 2026 wakati wa kutoa taarifa ya utendaji wa robo ya kwanza ya mwaka (Januari–Machi, 2026), ambapo alisema uingiliaji kati wa taasisi hiyo umeokoa hasara ya jumla ya Sh. 116,216,506 katika sekta ya elimu.  Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa, makadirio ya bei ya vifaa vya ujenzi wa madarasa hayo mawili yalikuwa chini ya bei halisi ya soko, hali iliyosababisha mfumo wa manunuzi wa kielektroniki wa Serikali (*NeST*) kukataa zabuni zote na kukwamisha maendeleo ya wan...