Serikali imeahidi kuchukua hatua za kudumu kukabiliana na tatizo la mmomonyoko wa ardhi na mafuriko yanayosababishwa na Korongo la Starehe katika Jimbo la Tarime Mjini, mkoani Mara. Kauli hiyo imetolewa leo Juni 10, 2026, Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Festo Dugange, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Esther Matiko, kuhusu hatua za Serikali kudhibiti korongo hilo ambalo limeendelea kuhatarisha maisha, mali na makazi ya wananchi. Dkt. Dugange amesema Serikali imeweka kipaumbele katika kuondoa maeneo hatarishi na kuboresha miundombinu ya kudhibiti mafuriko na mmomonyoko wa ardhi katika maeneo mbalimbali nchini. "Tutafanya tathmini ya kina kubaini sababu zinazofanya korongo hili kuendelea kuharibika licha ya jitihada zilizowahi kufanyika, na tutachukua hatua za kitaalamu kuhakikisha suluhisho la kudumu linapatikana," amesema. Aidha, ameelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Mara pamoja na Meneja wa TARURA Tarime Mjini ...
Marato tv - Sauti ya Jamii