NA: MWANDISHI WETU, PANGANI Timu zote 16 zilizoshiriki mashindano ya mpira wa miguu ya Aweso Vijana Cup 2026, zimeneemeka kushiriki mashindano hayo. Hii inatokana na uamuzi mfadhili wa mashindano hayo ambaye ni Mbunge wa Pangani na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kuamua kupeleka tabasamu kwa timu zote. Katika hotuba yake aliyoitoa Mei 16, 2026, katika uwanja wa Kumba wilayani Pangani, siku ya fainali iliyozikutanisha timu za Kata za Bweni na Kimang'a, Aweso ameahidi kuzipa zawadi timu zote zilizoshiriki mashindano hayo. "Ndugu zangu, nazipongeza timu za Bweni na Kimang'a kwa mechi nzuri iliyokuwa na ushindani mkubwa katika fainali hii. Pamoja na hayo, naahidi kuzipa timu zote zilizoshiriki mashindano haya shilingi 500,000, jezi seti moja na mpira ili kuendeleza kukuza michezo wilayani kwetu," amesema Aweso. Maamuzi haya ni motisha kwa wachezaji wa timu zilizoshiriki mashindano hayo kuendelea kucheza kwa bidii ili kukuza vipaji vyao. Katika mashindano hayo, timu 16 zili...