Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Kanali Evans Alfred Mtambi, leo tarehe 24 Disemba, amewatakia heri ya Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya wananchi wa Mkoa wa Mara, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara. Mheshimiwa Mtambi amesema anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuendelea kuwajaalia Watanzania, ikiwemo wananchi wa Mkoa wa Mara, afya njema hadi kufikia mwisho wa mwaka na kipindi cha sikukuu. Ameeleza kuwa kwa muda wote Mungu amekuwa karibu na Taifa kwa kulijalia amani na usalama, pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi zilizowawezesha wananchi kujipatia kipato kwa mwaka mzima. Hivyo, amewahimiza wananchi kutumia kipindi hiki cha sikukuu kumtukuza Mungu kwa kuwafikisha salama mwisho wa mwaka. Sambamba na hayo, Mheshimiwa Kanali Mtambi amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Mara kwa kuwahakikishia kuwa mkoa uko salama, hivyo waendelee kusherehekea sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya kwa amani na utulivu. Amesisitiza umuhimu wa wananchi kulinda afya zao na...
Marato tv - Sauti ya Jamii