Skip to main content

Posts

Showing posts from August 15, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tanzania yapongezwa Kuongoza Juhudi za Kutafuta Amani, SADC

Tanzania imepongezwa kwa utendaji mzuri wa kushughulikia changamoto za kiusalama katika kanda ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC),  baada ya kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Pongezi hizo zimetolewa Agosti 15, 2025, wakati wa Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama unaofanyika Madagascar chini ya mwenyekiti wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo.  Katika hotuba yake ya ufunguzi, Balozi Kombo alisema katika uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Tanzania iliongoza juhudi za pamoja za kutafuta ufumbuzi wa migogoro ya kikanda, kuimarisha utawala wa kidemokrasia na kuimarisha miongozo ya kulinda amani.  Hayo yalifanyika chini ya uongozi imara wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama. Katika kipindi cha mwaka mmoja, Tanzania iliitisha mikutano mitano ya dharur...

Waziri Wa Ulinzi na Jkt Afunga Mafunzo ya Jeshi la Akiba Mkoa Mwanza

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 15 Agosti 2025, amehitimisha kwa kufunga Mafunzo ya Jeshi la Akiba Mkoa Mwanza, shughuli iliyofanyika katika viwanja vya Mwanankanda wilayani Magu. Akitoa hotuba yake wakati wa Ufungaji Mafunzo hayo, Dkt. Tax amewataka wahitimu hao kutumia vizuri maarifa na weledi walioupata katika mafunzo hayo ili kukidhi matarajio ya Taifa na malengo ya misingi ya majukumu ya Jeshi la Akiba. Aidha, amewataka kudumisha nidhamu, Uzalendo na Uhodari katika utekelezaji wa majukumu yao huku wakifahamu kwamba Jeshi la Akiba ni sehemu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.  Akatamatisha kwa kuwakumbusha Wahitimu na Watanzania kushiriki Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba 2025, ili kuchagua Viongozi wanaoona watawafaa kuwaletea Maendeleo. Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya Magu, Mhe Jubilate Lawuo, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza, amemshukuru Waziri wa Ulinzi na JKT kwa kukubali kuwa Mgeni rasmi katika ufungaji wa M...

Wawekezaji Waitikia Wito wa Rais Samia wa Uongezaji Madini Thamani Nchini

▪️Waziri Mavunde azindua Kiwanda cha kuongeza thamani madini Chumvi-Kigoma ▪️Ni cha uzalishaji Chumvi Lishe(𝐶𝑎𝑡𝑡𝑙𝑒 𝐿𝑖𝑐𝑘) kwa ajili ya Mifugo ▪️Lengo ni kupunguza uagizaji wa Chumvi Lishe kutoka nje ya Nchi ▪️Tanzania kuongeza uzalishaji wa Chumvi ghafi kwa matumizi ya viwandani Uvinza,Kigoma Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Nyanza Salt kwa kuitikia wito wa Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan wa uongezaji thamani madini nchini kwa kuanza rasmi uzalishaji wa chumvi lishe itokanayo na madini ya Chumvi mahususi kwa ajili ya kuongeza virutubisho vya mifugo. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Wilayani Uvinza-Kigoma wakati akizindua shughuli za Kiwanda cha kuzalisha chumvi lishe(𝘾𝙖𝙩𝙩𝙡𝙚 𝙇𝙞𝙘𝙠) kwa ajili ya mifugo kinachomilikiwa na Kampuni ya Nyanza Salt. “Ni wito wa Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan na matakwa ya sheria juu ya uongezaji thamani madini yetu hapa nchini. Nawapongeza Kampuni ya Nyanza kwa hatua hii kubwa ya kuitoa chumvi yetu katika matumizi ya...

Mwenge wa Uhuru Waanza Mbio Zake Mkoani Mara

 Na Ada Ouko, Bunda. MKOA wa Mara unatarajia kukimbiza Mwenge wa uhuru takriban kilometa 1123 katika wilaya sita na Halmshauri tisa za mkoa huo, sambamba na kuweka mawe ya msingi kuzindua na kufungua miradi 68 ya maendeleo ya wananchi yenye thamani ya shilingi Bilioni 26.5 Hayo yamebainishwa Agosti 15,2025 na Katibu tawala wa Mkoa huo Gerald Kusaya wakati akipokea Mwenge huo kutoka kwa Katibu tawala wa mkoa wa Simiyu Prisca Kayombo, Makabidhiano hayo yamefanyika wilayani Bunda mkoani humo. "Mkoa wa Mara umejipanga kushiriki mbio za Mwenge wa uhuru kikamilifu ambapo katika mbio hizo utatembea kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi ya maendeleo ya wananchi 68 . yenye thamani ya shilingi 26.5 ambapo miongoni mwa miradi hiyo ni sekta za Afya,Maji, Elimu, Ujenzi,Kilimo, Mifugo, Mazingira, Ustawi wa jamii, Viwanda na Biashara" alisema Gerald. Aidha amesema Mwenge huo ulioasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julias Nyerere utakapopita wilaya ya Butiama utapata nafasi ya kuwasha m...