CCM Mara Yaridhishwa na Utendaji Kazi wa Tanroads Mkoa Katika Utekelezaji na Usimamizi wa Miradi ya Barabara
Na Shomari Binda-Musoma CHAMA cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mara kimedai kuridhishwa na utendaji kazi, utekelezaji na ufatiliaji miradi ya barabara inayofanywa na Wakala wa Barabara Tanroads mkoa wa Mara. Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa CCM mkoa wa Mara Ibrahim Mjanakheri alipokuwa akizungumza na George Marato TV kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika ofisini kwake. Amesema serikali ya awamu ya Sita chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassan, imefanya kazi kubwa kuleta fedha za miradi ya maendeleo na mkoa wa Mara umenufaika. Katibu huyo amesema eneo la miundombinu ikiwemo ya barabara imepata fedha na Tanrods mkoa wa Mara imefanya kazi nzuri katika kusimamia na miradi inaendelea vizuri. Amesema katika kipindi cha mvua barabara zote zilikuwa zikipitika na hakuna taarifa yoyote iliyolipotiwa ya barabara kushindwa kupitika kwa kukatika Mjanakheri amesema hali hiyo ni kuonyesha Tanrods mkoa wa Mara inatekeleza vizuri majukumu yake kupitia usimamizi wa meneja wa mkoa mhandisi Vedastus M...