WAZIRI MAVUNDE ATOA WITO WAMILIKI WOTE WA LESENI ZA UCHIMBAJI WA MADINI KINYWE KUANZA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MARA MOJA
■ Lengo ni kuifanya Tanzania kuwa kinara wa uzalishaji wa madini kinywe ifikapo Mwaka 2030 ■ Serikali yasaini mkataba wa ubia na Kampuni za Grafica na Eminent. ■ Aitaka Timu ya majadiliano ya serikali kuanza mchakato wa majadiliano na Wamiliki wa Leseni 27 ■ Amshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha sekta ya madini, ■ Ruangwa kuwa sehemu ya mnyororo wa thamani na teknolojia ya madini kinywe duniani. *Ruangwa, Lindi* Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* ameielekeza Timu ya Majadiliano ya Serikali kwenye Sekta ya Madini (GNT) kuwaita na kufanya nao majadiliano wamiliki wote wa leseni za uchimbaji madini kinywe nchini Tanzania kujadiliana kuhusu ubia wa serikali katika Kampuni hizo na kuwataka kuanza utekelezaji wa uchimbaji kwa mujibu wa masharti ya leseni na Sheria ya Madini Sura ya 123. Ameyasema hayo leo tarehe 30 Mei, 2026 Wilayani Ruangwa aliposhiriki zoezi la utiaji saini na Kampuni za Grafica Resources na Eminent Minerals Limited zenye ubia wa...