▪️Ni Leseni Hodhi zilizorudi Serikalini baada ya kumalizika kesi na wawekezaji ▪️Mapato ya Serikali kuongezeka kupitia mrabaha na kodi mbalimbali ▪️ Waziri Mavunde asisitiza kuongeza utafiti zaidi ili kuongeza uzalishaji wa dhahabu ▪️Wachimbaji wadogo nao wapatiwa Leseni kuongeza uzalishaji 📍 *Chunya- Mbeya* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amezindua rasmi shughuli za uchimbaji madini katika mgodi wa Porcupine North- uliopo Makongorosi Wilayani Chunya Mkoa wa Mbeya unaomilikiwa na Kampuni ya Shanta Gold Mining Limited na kusema kuwa hatua hiyo ni matunda ya uamuzi wa Serikali kurudisha leseni ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha unawekwa utaratibu mzuri wa kuongeza mapato ya nchi kupitia sekta ya madini. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Aprili 03, 2025 katika hafla ya Uzinduzi wa Shughuli za Uchimbaji Madini Porcupine North – Kata ya Mkola, Makongorosi Wilayani Chunya Mkoa wa Mbeya. “Eneo hili ni eneo ambalo Leseni hodhi zimerudi se...
Marato tv - Sauti ya Jamii