Skip to main content

Posts

Showing posts from July 12, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

IMF YAIPATIA TANZANIA DOLA ZA MAREKANI MILIONI 444 KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA KIMKAKATI

 Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), limeidhinisha kutolewa mara moja kwa takriban dola za Marekani milioni 443.9 kwa Tanzania baada ya kukamilisha tathmini za mwisho chini ya programu za Extended Credit Facility (ECF) inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii na Resilience and Sustainability Facility (RSF) ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Katika taarifa iliyotolewa Julai 10, IMF imesema uamuzi huo unafuatia kukamilika kwa mapitio ya sita na saba ya mpango wa ECF pamoja na mapitio ya tatu na nne ya mpango wa RSF, ambapo fedha hizo zinajumuisha takriban dola za Marekani milioni 158.75 chini ya ECF na dola za Marekani milioni 298.37 chini ya RSF. IMF imeeleza kuwa uchumi wa Tanzania umeendelea kuonyesha uimara, huku ukuaji wa Pato la Taifa ukifikia asilimia 5.9 mwaka 2025 na kutarajiwa kufika karibu asilimia 6.2 kwa muda wa kati. Sekta zilizotajwa ...

GOVERNMENT APPLAUDS TANZANIA'S FIRST EV FACTORY

 The Government has commended Plug & Ride Tanzania for establishing the country's first electric vehicle manufacturing plant, describing the investment as a significant milestone that represents innovation, technology transfer, skills development, and the growth of Tanzania's industrial sector. The company is the result of a partnership between India's Mangal Eco Group and Tanzania's Utegi Group. This collaboration demonstrates what can be achieved when two friendly nations combine their strengths, expertise, and shared vision for sustainable development. The commendation was delivered in Dar es Salaam by the Deputy Minister for Transport, David Kihenzile, during the official launch of Plug & Ride Tanzania on behalf of the Minister for Transport, Professor Makame Mbarawa. "Today, Plug & Ride Tanzania is another important example of this long-standing partnership. Through this collaboration, the company has brought together India's technological exce...

WANANCHI WAJIFUNZA KUTAMBUA UBORA WA MADINI YA VITO

 📍Dar es Salaam Wananchi wanaotembelea banda la Tume ya Madini katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SabaSaba) wanaendelea kunufaika na elimu kuhusu matumizi ya kifaa cha Gemmological Torch, kinachotumika kutambua ubora na thamani halisi ya madini ya vito. Akitoa elimu katika banda hilo, Mjiolojia na Mjimolojia Mwandamizi kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mirerani, Selemani Khamisi, amesema thamani ya madini ya vito hupimwa kwa kuzingatia vigezo vinne vikuu vinavyojulikana kitaalam kama 4Cs, ambavyo ni rangi (Colour), uzito (Carat), ubora (Clarity) na umbo la ukataji (Cut). Amesema pamoja na matumizi ya Gemmological Torch, wataalam pia hutumia vifaa vingine vya kitaalam ikiwemo Head Loupe, Table Lamp na Price Guide ya Serikali ili kufanya tathmini ya kina ya ubora wa jiwe.  Uchunguzi huo huwezesha kubaini nyufa, mipasuko, uchafu wa ndani (inclusions), pamoja na ubora na ukolezi wa rangi ya jiwe. “Kadiri jiwe linavyokuwa na rangi ang’avu, ubora mzur...

DKT. MWIGULU ATAKA USHIRIKIANO WA KITAIFA KULINDA AMANI

   Na. Mwandishi Wetu - Dar es Salaam SERIKALI imewataka Watanzania kuendelea kulinda na kudumisha amani ya nchi kwa kutambua kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa, huku ikisisitiza kuwa jukumu hilo linamhusu kila mwananchi bila kujali dini, kabila au itikadi za kisiasa. Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, profesa Palamagamba Kabudi, wakati wa Ibada ya Siku Maalumu ya Wanaume (AMO Big Day) iliyofanyika katika Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA), Mwenge, tarehe 11 Julai, 2026 jijini Dar es Salaam. Dkt. Nchemba alisema ulinzi wa amani unapaswa kupewa kipaumbele na kuwa ajenda namba moja ya kitaifa kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, unaowezesha wananchi kuishi kwa utulivu, kufanya kazi kwa bidii na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa. Alisema kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda amani kwa kuheshimu ...

DKT. MWIGULU ATAKA USHIRIKIANO WA KITAIFA KULINDA AMANI

 Na. Mwandishi Wetu - Dar es Salaam SERIKALI imewataka Watanzania kuendelea kulinda na kudumisha amani ya nchi kwa kutambua kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa, huku ikisisitiza kuwa jukumu hilo linamhusu kila mwananchi bila kujali dini, kabila au itikadi za kisiasa. Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, profesa Palamagamba Kabudi, wakati wa Ibada ya Siku Maalumu ya Wanaume (AMO Big Day) iliyofanyika katika Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA), Mwenge, tarehe 11 Julai, 2026 jijini Dar es Salaam. Dkt. Nchemba alisema ulinzi wa amani unapaswa kupewa kipaumbele na kuwa ajenda namba moja ya kitaifa kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, unaowezesha wananchi kuishi kwa utulivu, kufanya kazi kwa bidii na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa. Alisema kila Mtanzania ana wajibu wa kulinda amani kwa kuheshimu sheria ...

SERIKALI YAPONGEZA UWEKEZAJI WA KAMPUNI YA PLUG&RIDE ZA TANZANIA NA INDIA

 Katika hatua za kukuza Sekta ya Usafirishaji na Utatuzi wa changamoto katika jamii, Wizara ya Uchukuzi imeipongeza kampuni ya UTEGI Limited kwa kufanikisha uwekezaji katika nyanja ya usafirishaji kupitia Kampuni ya Plug & Ride Tanzania iliunganisha maitaifa ya Tanzania na India.  Akizungumza mapema hii leo, Naibu Waziri, Wizara ya Uchukuzi Mhe. David M. Kihenzile kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi , Profesa Makame Mbarawa, wakati aliposhiriki katika hafla ya Uzinduzi wa kampuni ya Plug & Ride Tanzania, inayojihusisha na usambazaji na uundaji wa vyombo vya usafiri vinavyotajwa kwenda kupunguza hadha ya kubebea wagonjwa na watoto wa shule katika hospitali na shule mbalimbali nchini. Aidha, Amepongeza ujio wa uwekezaji huo ambapo amesema utaenda kuchangia uchumi wa Taifa, ikiwa ni pamoja na kuendeleza sera ya utunzaji mazingira kwa matumizi ya umeme pamoja na kuongeza idadi ya ajira kwa vijana wa kitanzania. Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. A...