Skip to main content

Posts

Showing posts from February 8, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hivi Ndivyo Alivyouawa Mtoto wa Gaddafi

 Ripoti ya awali ya uchunguzi kuhusu kuuwawa kwa Saif Al-islam Gaddafi imetolewa mapema leo asubuhi baada uchunguzi uliofanyika kutokana na uchunguzi wa kina wa kitabibu "Autopsy". Ripoti hiyo imetolewa na kamati ya uchunguzi ya bunge, inaonesha kuwa Idadi ya risasi zilizoingia kwenye mwili wa Saif Al-islam Gaddafi zilikuwa risasi 19, na risasi zilizotolewa mwilini kwake zimeonesha silaha iliyotumika katika mauaji yake ni silaha aina ya Kalashnikov, ni siraha ya kirusi. Moja ya risasi zilizo mpata ni pamoja na iliyo penya kichwani kwa Saif Al-islam Gaddafi, ambayo ilimpiga juu ya nyusi yake, yani juu ya jicho la kushoto na kutokae kwa nyuma. Muda ambao mashambulizi ya mauaji yake yaliyo pelekea kifo chake ilikuwa ni saa 05:57 PM saa za Libya. Kabla nyumba yake kuvamiwa na wauaji kwanza, saa moja na nusu nyuma walinzi wake wote waliondolewa karibu na makazi yake Saif Al-islam, na kubakia yeye pekee yake. Yani saa moja na nusu kabla ya tukio la uvamizi kutokea walinzi wote wali...

Balozi Matinyi akutana na wawekezaji wa Sweden, aelekezea fursa za uwekezaji

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, ameongoza ujumbe wa ubalozi na taasisi za Serikali ya Tanzania katika kikao cha kimkakati na wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Chama cha Wafanyabiashara wa Sweden na Afrika, kilichofanyika tarehe 6 Februari, 2026, katika  Ubalozi wa Tanzania jijini Stockholm, Sweden.  Kikao hicho kiliandaliwa mahsusi kwa ajili ya kuelezea fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini, pamoja na kufafanua mazingira bora ya uwekezaji yaliyowekwa na Serikali. Ujumbe wa Sweden uliongozwa na rais wa chama hicho, Bi. Ã…sa Jarskog, ambapo kwa Tanzania mbali ya Ubalozi zilikuwepo pia taasisi za Serikali zilizoshiriki kwa njia ya mtandao kutokea jijini Dar es Salaam.  Taasisi hizo ambazo zilitumia fursa hiyo kufafanua masuala kadhaa zilikuwa ni Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BR...

Prof.Shemdoe amshukuru Rais Dkt Samia kwa kurejesha Tabasamu kwa Wafabiashara Kariakoo

Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Shingi Bilioni 28 zilizorejesha tabasamu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo ambazo zimetumika kujenga Soko Jipya la Kariakoo na kukarabati Soko la zamani la Kariakoo ambalo liliharibika kutokana na janga la moto  Oktoba 07, 2021. Prof. Shemdoe ametoa shukrani hizo leo kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akitoa neno la utangulizi, wakati ya hafla ya ufunguzi wa Soko Kuu Jipya la Kariakoo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.  “Mhe. Rais natumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kwa nia yako njema ya kurejesha tabasamu kwa wafanyabishara na wananchi, kwa kutoa fedha zaidi ya  Shilingi Bilioni 28 ili kujenga soko jipya na kukarabati lililoteketea kwa janga la moto la Oktoba 07, 2021”, ameeleza Prof. Shemdoe. Prof. S...

Makamu Kwenyekiti Wa Ccm Tanzania Bara Akutana na Waziri wa Fedha

  Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM-Taifa, Mhe. Stephen Wasira, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), aliyefika kujitambulisha katika Ofisi za CCM, Lumumba, Jijini Dar es Salaam, baada ya hivi karibuni kuteuliwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasssan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.