▪️Kiasi cha tani milioni 139 ya mashapo ya urani yakadiriwa kuwapo,* ▪️Madini ya Urani kutumika kuzalishia umeme nchini ▪️ Rais Samia apongezwa kwa kuvutia uwekezaji ▪️Ujenzi wa kiwanda cha majaribio cha uchenjuaji wa Urani wakamilika ▪️Mradi kugharimu Trilioni 3.06 mpaka kukamilika kwake Namtumbo,Ruvuma Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* abainisha kuwa mradi wa kimkakati wa uchimbaji wa madini ya Urani kuanza hivi karibuni baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kiwanda cha majaribio cha uchenjuaji wa madini hayo. Ameyasema hayo jana tarehe 18 Julai, 2025 Wilayani Namtumbo alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo unaokadiriwa kugharimu zaidi ya Tsh 3.06 Trilioni unaotekelezwa na Kampuni ya Mantra Tanzania Limited. "Moja kati ya vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa *Mhe. Dkt. Samia S.Hassan* kwenye sekta ya madini ni suala la uongezaji thamani madini ndani ya nchi yetu, na Mhe. Rais ametupa maelekezo mahsusi Wiz...
Marato tv - Sauti ya Jamii