Makatibu Wakuu wa Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanaosimamia masuala ya mtangamano wamekutana katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha, ikiwa ni muendelezo wa maandalizi ya Mkutano wa 25 Wakuu wa Nchi Wanachama wa EAC utakaofanyika tarehe 7 Machi 2026 jijini Arusha. Kikao hicho cha Makatibu Wakuu ambacho ni sehemu ya Mkutano Maalum wa 59 wa Baraza la Mawaziri wa EAC, pamoja na masuala mengine umepokea na kujadili agenda na taarifa mbalimbali zilizowasilishwa na mkutano wa Ngazi ya Wataalamu uliofanyika tarehe 2 hadi 3 Machi 2026. Agenda na taarifa hizo zitawasilishwa na kujadiliwa kwenye Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 5 Machi 2026 jijini Arusha. Akifungua mkutano huo Dkt. Caroline W. Karugu PhD, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki nchini Kenya, na Mwenyekiti wa mkutano huo, ameeleza kuwa Jumuiya imeendelea kupiga hatua kubwa ya maendeleo huku ikizingatia ustawi wa watu wake kwa kuwezesha shughuli mbalimbali za...
Marato tv - Sauti ya Jamii