Chuo Kikuu cha Makerere kimepanga Kugeuza Hosteli zake kuwa Hoteli wakati wa Likizo ya Wanafunzi ili kuongeza Mapato ya chuo hicho kikongwe zaidi Afrika Mashariki. Mpango huo umebainishwa Julai 25,2025 na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Barnabas Nawangwe wakati wa Makabidhiano ya Moja ya Hosteli iliyofanyiwa ukarabati mkubwa na wa kisasa. "Nadhani tunatumia vibaya Hosteli hizi,kwanini zikae bila kutumika kwa miezi yote mitatu wanafunzi wanapokuwa Likizo bila kuzalisha fedha ilhali Hosteli zetu ni Bora kuliko hata baadhi ya Hoteli" Alisema Profesa Nawangwe wakati wa Makabidhiano hayo. Profesa Nawangwe amesema kuwa Chuo hicho kitashirikiana na wafanyabiashara pamoja na kampuni yake ya Makerere Holding Ltd kwa ajili ya kusimamia uendeshaji wa hosteli hizo Kibiashara wakati wa Likizo. "Kwanini tusizigeuze hoteli wanafunzi wetu wanapokuwa Likizo, Watu wenye Mikutano wawe wanaleta washiriki hapa kupata huduma ya Malazi,pia wanaweza kufanyia Mikutano yao hapa na kutup...
Marato tv - Sauti ya Jamii