Skip to main content

Posts

Showing posts from May 5, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

REA Yawezesha Vikosi vya JKT Kukuza Matumizi ya Nishati Safi

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa vikosi vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) vilivyopata miradi ya nishati safi ya kupikia kuwa mabalozi wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa jamii zinazowazunguka. Mwenyekiti Kingu ametoa wito huo leo Mei 5, 2026 wakati wa ziara ya Bodi hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia inaayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika Kambi ya JKT ya Maramba mkoani Tanga. Aidha, amesisitiza vijana wanaliopo kwenye kambi hizo za JKT kupatiwa mafunzo ya namna ya kutengeneza mkaa mbadala ili waweze kutumia ujuzi huo kujiajiri na kuwa mawakala wa kutengeneza mkaa mbadala pindi watakapomaliza mafunzo yao. Kwa upande wake, akimwakilisha Mkuu wa JKT, Kanali Projest Rutaihwa aliishukuru menejimenti na Bodi ya REA kwa utekelezaji wa miradi nishati safi ya kupikia huku akiahidi kusimamia mradi huo unakuwa endelevu ili kuendelea kulinda mazingi...

Geita Regional Commissioner to Officiate Tanzania’s World Donkey Day 2026

By Prosper Makene Geita Regional Commissioner, Mr Martin Shigela will officiate this year’s national World Donkey Day celebrations on Friday, May 8, 2026, at Mgusu Ward in Geita Municipal Council.  The United Republic of Tanzania, through the Ministry of Livestock and Fisheries, is hosting the event to highlight the vital role donkeys play in rural livelihoods. The announcement was made yesterday by the Ministry in Dodoma through an official public notice, emphasizing the government’s commitment to animal welfare and rural development. Caring for Donkeys is Our Collective Responsibility This year’s theme underscores the economic and social value of donkeys across Tanzania and Africa. The theme was adopted following the African Union Heads of State Summit held in Dar es Salaam in October 2022. During that summit, 32 African nations officially recognized donkeys as critical to the continent’s transport, agriculture, and household economies, and pledged to strengthen protections again...

Mkuu wa Mkoa wa Geita Kufungua Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Punda Duniani 2026

Na Prosper Makene Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martin Shigela, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Punda Duniani yatakayofanyika Ijumaa, Mei 8, 2026, katika Kijiji Cha Mgusu, Kata ya Mgusu, Halmashauri ya Manispaa ya Geita. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, inaandaa tukio hilo kuangazia mchango mkubwa wa punda katika maisha ya vijijini. Tangazo hilo lilitolewa jana na Wizara jijini Dodoma kupitia taarifa rasmi kwa umma, likisisitiza dhamira ya Serikali katika ustawi wa wanyama na maendeleo ya vijijini. *Kumtunza Punda ni Jukumu la Sote*   Kaulimbiu ya mwaka huu inasisitiza thamani ya kiuchumi na kijamii ya punda nchini Tanzania na Afrika nzima. Kaulimbiu hiyo ilipitishwa kufuatia Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika uliofanyika Dar es Salaam mwezi Oktoba 2022. Katika mkutano huo, mataifa 32 ya Afrika yalitambua rasmi kuwa punda ni nguzo muhimu ya usafirishaji, kilimo, na uchumi wa kaya barani Afrika, na ...

MMI Yaimarishwa Misungwi: Wakuu wa Idara Wakumbushwa Umuhimu wa Kujibu Hoja za CAG

 Na Thomas Lutego ; Misungwi  Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi.Peniel Titus ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Mipango wa Halmashauri hiyo amefungua Mafunzo ya MMI na Amesisitiza Umuhimu wa Mafunzo Hayo kwa Wakuu wa Idara na Vitengo kwani ndio Sehemu za kujibu Hoja za CAG ambapo Mafunzo hayo ni Muhimu kwa Halmashauri Katika kutekeleza Shughuli mbalimbali za Miradi. Mkufunzi wa MMI Mkoa  wa Mwanza Bw. Kusire Swai ameeleza kuwa Mafunzo hayo ni Marefu hivyo yanahitaji Umakini Na Ufuatiliaji. Hivyo ni Vyema Kufuata Sheria,Kanuni,Taratibu na Miongozo na ni Muhimu Mafunzo haya Wapewe wakuu wa Idara na Vitengo  kwani Mafunzo haya ya hoja ni Muhimu  kwani chanzo cha hoja ni kuanzisha Mradi na ndio wahusika wa hoja. Amesisitiza kwa Sasa Hoja zote zitajibiwa kwenye Mfumo ambao Umeboreshwa na TAMISEMI.

Samia Aendeleza Diplomasia ya Michezo, Akutana na Didier Drogba Dodoma

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo akiwa Ikulu jijini Dodoma amekutana na nyota wa zamani wa klabu ya Chelsea F.C. na Timu ya Taifa ya Ivory Coast, Didier Drogba, pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda. Mkutano huo unaangaliwa kama sehemu ya kuimarisha diplomasia ya michezo (sports diplomacy), ambapo ushirikiano kati ya serikali na mastaa wa kimataifa unatumika kukuza sekta ya michezo kama kichocheo cha ajira, uwekezaji na utalii wa michezo nchini.

Serikali Yaimarisha Huduma ya Maji Kwa Asilimia 85.2 Vijijini, 92.5 Mijini

WAZIRI wa Maji, Juma Aweso, amesema Serikali inaendelea kupiga hatua katika upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi, ikilenga kufikia asilimia 90 vijijini na asilimia 95 mijini ifikapo mwaka 2030. Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2026/2027 Bungeni leo Mei 5, 2026, Aweso alisema hadi Desemba 2025, huduma ya maji vijijini imefikia asilimia 85.2 kutoka asilimia 83.1 mwaka 2024. Mafanikio hayo yametokana na kukamilika kwa miradi 54 yenye vituo 946 vya kuchotea maji, vilivyonufaisha wananchi zaidi ya 493,932 katika vijiji 151. Kwa mujibu wa Aweso, Amesema hatua hiyo imeongeza idadi ya wananchi wa vijijini wanaopata huduma ya maji kufikia zaidi ya milioni 38.6. Kwa upande wa mijini, upatikanaji wa maji umefikia asilimia 92.5 hadi Desemba 2025, ukiongezeka kutoka asilimia 90.6 mwaka uliopita.  "Hali hii imechangiwa na kukamilika kwa miradi 12 inayohudumia watu 880,633, huku miradi mingine 214 ikiendelea kutekelezwa". Amesema Kuhusu usafi wa mazingira,...

Wizara ya Maji Yatoa Vipaumbele na Mwelekeo wa Sekta ya Maji 2026/2027

WIZARA ya Maji imewasilisha vipaumbele na mwelekeo wa sekta ya maji kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ikiwa ni mkakati wa Serikali kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama unaongezeka nchini kote, hususan vijijini na mijini. Akizungumza leo Mei 5,2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maji Kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 Waziri wa Maji, Mhe. Juma Aweso amesema Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji ili kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi wote na kuendana na mahitaji ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. “Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa wananchi na shughuli za maendeleo,” amesema Mhe. Aweso. Wizara imesema itaendelea na utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Taifa wa Maji pamoja na Gridi ya Taifa ya Maji ambayo inalenga kusafirisha maji kutoka vyanzo vikuu kama maziwa na mito kwenda maeneo yenye uhaba mkubwa wa maji nchini. Katika kuongeza uhakika wa m...

Rais Ruto:Ondoeni Vikwazo, Wafrika Mashariki ni Wamoja Tayari

RAIS wa Kenya, William Samoei Ruto, ametoa wito kwa nchi za Afrika Mashariki kuondoa vikwazo vinavyokwamisha uhuru wa usafiri wa watu, bidhaa na huduma, akisisitiza kuwa mshikamano wa kikanda haupaswi kuzuiliwa na mipaka ya kisiasa. Akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  jijini Dodoma leo Mei 5, 2026, katika hitimisho la ziara yake ya kikazi ya siku mbili nchini Tanzania, Ruto amesema uhalisia wa maisha ya wananchi wa Afrika Mashariki tayari unaonesha umoja wa dhati. “Wananchi wetu tayari wameunganishwa kupitia familia, biashara na shughuli za kiuchumi zinazovuka mipaka; ni wajibu wa sera zetu kuendana na hali hiyo,” amesema Ruto. Amebainisha kuwa kuna maelfu ya wananchi wenye ndugu pande zote za mipaka, huku wafanyabiashara na wajasiriamali wakitegemea usafirishaji rahisi ili kukuza shughuli zao za kiuchumi. “Hatuwezi kuzungumzia soko la pamoja huku tukidumisha vikwazo vinavyowazuia wananchi na bidhaa zao kusafiri kwa uhuru,” ameongeza. Akitoa mfano wa umoja wa asi...