Skip to main content

Posts

Showing posts from March 8, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa amwakilisha Rais Dkt.Samia ibada ya kumwekea Wakfu Rev.Canon Mlula.

  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Machi 09, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye ibada ya kumweka wakfu na kumweka kitini Rev. Canon Bethuel Joel Mlula kuwa askofu wa pili wa kanisa Anglikana, Dayosisi ya Kiteto. Ibada hiyo imefanyika katika Kanisa Kuu Anglikana na Mtakatifu Mikaeli, Kiteto.

Mwenyekiti Wa Ccm Kata ya Kamnyonge Amshukuru Mbunge Mathayo Utekelezaji wa Ahadi ya Viti

Na Shomari Binda-Musoma  MWENYEKITI wa chama cha Mapinduzi ( CCM) Kata ya Kamnyonge Emanuel Bwimbo amemshukuru mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo kwa kutekeleza ahadi yake ya kuwapa viti 50. Ahadi hiyo imetekelezwa leo machi 8/2025 na Katibu wa mbunge huyo Christopher Majala kwenye ofisi za chama hicho Kata ya Kamnyonge. Akipokea viti hivyo Mwenyekiti huyo amesema kutokana na upungufu wa viti kwenye ofisi yao walifikisha ombi kwa mbunge machi 3/2025 alipofanya ziara ya kuitembelea Kata hiyo na kwa muda mfupi ameitekeleza. Amesema licha ya maombi ya viti ambavyo tayari wamevipata walitoa maombi ya kukarabatiwa kwa jengo la ukumbi ambao pia ameahidi kuanza ukarabati wake hivi karibuni. Bwimbo amesema ilikuwa ikiwapelekea kukodisha viti wanapotaka kufanya vikao lakini kwa sasa adha hiyo itakuwa haipo kutokana na mbunge kuwashika mkono. " Tunamshukuru sana mheshimiwa mbunge Mathayo kwa leo kutekeleza ahadi yake ya viti baada ya kufikisha maombi kwake. " Ni juzi alit...

Rais Samia: Tanzania imepiga Hatua Kubwa Katika Usawa wa Kijinsia

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kupitia utekelezaji wa Ilani ya CCM, Serikali imepiga hatua kubwa katika kufanikisha malengo ya kuhakikisha kesho bora na njema zaidi kwa vijana wa Kitanzania, wa kike na wa kiume. Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mwanamke, yaliyofanyika leo Jumamosi, tarehe 8 Machi 2025, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, Mhe. Rais Dkt. Samia alieleza kuwa Tanzania ina mengi ya kujivunia katika kuboresha mazingira yanayohakikisha ndoto ya usawa wa kijinsia inafikiwa nchini. “Tunapoadhimisha miaka 30 tangu Tamko la Umoja wa Mataifa la Mkutano wa Beijing, miaka 10 ya Malengo Endelevu ya Dunia na miaka 5 ya Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa, ni fursa ya kutathmini mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kutambua hatua zaidi zinazohitajika ili kuhakikisha kila msichana na mwanamke hapa nchini anapata nafasi ya kufikia ndoto zake,...

Watumishi Wanawake Takukuru Mara Watembelea Watoto yatima Tarime na Kutoa Misaada

  Na Shomari Binda-Tarime  WATUMISHI wanawake wa Taasisi  ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)mkoa wa Mara wametembelea kituo cha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu cha 'Angel House' kilichopo katika Wilaya ya Tarime na kutoa misaada ya vitu mbalimbali. Katika tukio hilo la matendo ya huruma  TAKUKURU imewapatia watoto hao mahitaji muhimu yakiwemo vyakula, mavazi na vifaa vya shule . Akizungumza baada ya kukabidhi misaada hiyo,Afisa wa TAKUKURU mkoa wa Mara Restituta Kessy amesema katika kusherehekea siku ya kimataifa ya wanawake duniani wameona wawafikie watoto hao kwenye kituo hicho. Amesema ni jambo la faraja kumuona kila mtoto anakuwa na furaha wakiwemo watoto yatima na kujiona kama watoto wengine. Afisa huyo amesema jamii inapaswa kuwa na utaratibu wa kutembelea vituo vya watoto yatima na wenye uhitaji ili kuweza kuwasaidia na kuwafanya kuwa na furaha. Amesema zipo baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu pale unapowasaidia watoto yatima na wenye ...

Dc Chikoka Azindua Utoaji Huduma Za Afya Kituo Kipya Musoma Vijijini

  Na Shomari Binda-Musoma  MKUU wa Wilaya ya Musoma Juma Chikoka amezindua utoaji wa huduma za afya kwenye kituo kipya cha afya cha Kata ya Makojo chenye Vijiji 3 vya Chimati, Chitare na Makojo) Jimbo la Musoma Vijijini linaendelea kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma za afya ndani ya Kata zake 21 zenye jumla ya vijiji 68. Akizungumza jana machi 6/ 2025 wakati wa uzinduzi huo mkuu huyo wa Wilaya amesema suala la afya kwa wananchi ni suala la msingi kwani afya bora inamfanya mwananchi kutekeleza vyema majukumu yake. Amesema serekali ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imekuwa ikifanya jitihada kubwa kuboresha utoaji wa huduma za afya na Musoma Vijijini imekuwa ikifikiwa na huduma hizo. Chikoka amesema watoa huduma wanapaswa kuzingatia maadili ya utoaji huduma nzuri kwa wananchi kuanzia kwenye zahanati,vituo vya afya na hospital. Amesema sio vyema kuona wananchi wakilalamikia huduma wakati serikali imejenga kituo cha afya na kupeleka vifaa tiba na dawa. Kwa upande wa taarifa ili...

Askari Wanawake wa Vyombo Vya Ulinzi Nchini Walivyopamba Siku ya Wanawake

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 08 Machi, 2025. Maandamano ya Wanawake kutoka Taasisi mbalimbali za umma na binafsi yakipita mbele ya Jukwaa kuu kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 08 Machi

Vijana wenye elimu ya dini ni nguzo muhimu ya maendeleo - Majaliwa.

  WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema vijana wenye elimu na maarifa ya dini ni nguzo muhimu ya ustawi na maendeleo katika jamii kwani imani imara ya kidini hujenga jamii zenye maadili mema, ufanisi katika kazi, na upendo wa dhati kwa kila mmoja. Pia, Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali ina matarajio makubwa kwa vijana wanaoshiriki mashindano Quran kwani kwa kutumia maarifa na ujuzi wanaoupata katika mashindano hayo kutekeleza majukumu muhimu ya kijamii na kiroho metoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Machi 8, 2025) alipozungumza na wananchi katika Mashindano ya 16 ya Kuhifadhi Quran Tukufu ngazi ya Afrika Mashariki na Kati yaliyofanyika katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi, Dar es Salaam. “Mashindano haya ni fursa ya kukuza imani na maarifa yenu. Kuhifadhi Quran ni jambo lenye manufaa mengi kwani inaimarisha uhusiano wenu na Mwenyezi Mungu na inajenga msimamo wa kiroho. Nina hakika mnapokuwa na imani imara, nidhamu, na maadili mazuri baadaye mtakuwa viongozi bora wa familia, jamii, na...